Yehoshafati (kwa Kiebrania: יְהוֹשָׁפָט, Yəhōšafat, Yŏhōšāp̄āṭ[1], Mungu amehukumu; 905 KK hivi - 849 KK hivi) alitawala ufalme wa Yuda kati ya miaka 870 KK na 849 KK.

Mfalme Yehoshafati alivyochorwa na Guillaume Rouillé mwaka 1553.

Muda huo alijitahidi kurudisha Israeli kwa Mungu pekee, YHWH, kama alivyofanya baba yake Asa.

Habari zake zinapatikana hasa katika Kitabu cha Pili cha Wafalme 15-22 na Kitabu cha Pili cha Mambo ya Nyakati 17-21.

Pia anatajwa na Injili ya Mathayo kati ya mababu wa Yesu Kristo.

Tanbihi hariri

  1. Khan, Geoffrey (2020). The Tiberian Pronunciation Tradition of Biblical Hebrew, Volume 1. Open Book Publishers. ISBN 978-1783746767. 

Viungo vya nje hariri

  Makala hii kuhusu mtu wa Biblia bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Yehoshafati kama habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.