Anatolia
Anatolia (Kituruki: Anadolu) ni rasi kubwa katika Asia ya Magharibi kati ya Bahari ya Mediteranea na Bahari Nyeusi. Eneo lake ni sehemu kubwa ya Uturuki upande wa Asia.
![](http://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/thumb/d/db/Turkey_topo.jpg/400px-Turkey_topo.jpg)
Jina la Kale ni "Asia Minor" (kilat.) au " Asia Ndogo".
Katika historia mataifa mengi yaliishi Anatolia au kuingia humo na kujenga madola yao kama vile Wahitti, Wagiriki, Wajemi, Waarmenia, Waroma, Wagothi, Wabizanti na Waturuki.