Ario (kwa Kiberberi: Aryus ; kwa Kigiriki Ἄρειος, Areios, 250 au 256336) alikuwa padri kutoka Libya aliyefanya kazi huko Alexandria, Misri.[1]

Mchoro wa Mtaguso wa kwanza wa Nisea ukimuonyesha Ario chini ya mihuu ya Kaisari Konstantino Mkuu na maaskofu.

Mafundisho yake[2][3] yalisisitiza kuwa Mungu Baba ni mkuu kuliko Mwana,[4] akipinga imani katika Utatu.[5]

Kristolojia yake ilikanushwa na askofu wake, Aleksanda wa Aleksandria, lakini ilienea kote mashariki mwa Dola la Roma na kuvuruga Kanisa Katoliki kiasi cha kudai Kaisari Konstantino I aitishe Mtaguso wa kwanza wa Nisea mwaka 325.

Huo mtaguso mkuu wa kwanza, uliokusanya maaskofu wengi hasa wa mashariki, ulikataa hoja zake na kumkiri Mwana kuwa na hali ileile ya Baba.

Hata hivyo vurugu ziliendelea hata kudai ufanyike mtaguso wa kwanza wa Konstantinopoli (383), ambao ni wa pili kati ya mitaguso ya kiekumene, nao ukasisitiza na kukamilisha imani ya mtaguso wa kwanza wa Nisea katika Kanuni ya Imani ya Nisea-Konstantinopoli.

Ingawa imani hiyo ilikubaliwa kura rasmi katika Dola la Roma, Uario ulienea kati ya makabila ya Kijerumani, hasa Wagoti na Wavandali, hivyo uliendelea hadi karne ya 7 na ya 8.

Mpaka leo kuna madhehebu yanayokanusha umungu wa Yesu Kristo na kusema ni kiumbe tu.

Maandishi yake hariri

Tanbihi hariri

  1. Anatolios, Khaled (2011). "2. Development of Trinitarian Doctrine: A Model and Its Application". Retrieving Nicaea. Grand Rapids: BakerAcademic. p. 44. ISBN 080103132X. Arius, who was born in Libya, was a respected ascetic and presbyter at the church of the Baucalis in Alexandria. 
  2. Hanson, R P C (2007). The Search for the Christian Doctrine of God. Grand Rapids: Baker Academic. pp. 127–128. ISBN 0-8010-3146-X. 
  3. Kopeck, M R (1985). "Neo Arian Religion: Evidence of the Apostolic Constitutions". Arianism: Historical and Theological Reassessments: 160–162. 
  4. Williams, Rowan (2002) [1987]. Arius (Revised ed.). Grand Rapids, Mich: W.B. Eerdmans. p. 98. ISBN 0-8028-4969-5. 
  5. Constantine the Great Rules Archived 21 Novemba 2017 at the Wayback Machine. - National Geographic - Retrieved 23 September 2014.

Marejeo hariri

  • Athanasi wa Aleksandria, History of the Arians, London, 2013. limovia.net ISBN 978-1-78336-206-6
  • Athanasi wa Aleksandria]]. History of the Arians. Online at CCEL. Part I Part II Part III Part IV Part V Part VI Part VII Part VIII. Accessed 13 December 2009.
  • Artemi, Eirini, The religious policy of the Byzantine emperors since the First to the Fourth ecoumenical council online onhttp://www.impantokratoros.gr/thriskeftikh-politikh.el.aspx
  • Ayres, Lewis. Nicaea and its Legacy: An Approach to Fourth-Century Trinitarian Theology. New York: Oxford University Press, 2004.
  • Hanson, R.P.C. The Search for the Christian Doctrine of God: The Arian Controversy, 318–381. T&T Clark, 1988.
  • Parvis, Sara. Marcellus of Ancyra And the Lost Years of the Arian Controversy 325–345. New York: Oxford University Press, 2006.
  • Rusch, William C. The Trinitarian Controversy. Sources of Early Christian Thought, 1980. ISBN 0-8006-1410-0
  • Schaff, Philip. "Theological Controversies and the Development of Orthodoxy". In History of the Christian Church, Vol III, Ch. IX. Online at CCEL. Accessed 13 December 2009.
  • Wace, Henry. A Dictionary of Christian Biography and Literature to the End of the Sixth Century A.D., with an Account of the Principal Sects a.d Heresies. Online at CCEL. Accessed 13 December 2009.
  • Williams, Rowan. Arius: Heresy and Tradition. Revised edition, 2001. ISBN 0-8028-4969-5
  Makala hii kuhusu dini ya Ukristo bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Ario kama historia yake, matokeo au athari zake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.