Aleksanda I wa Aleksandria

(Elekezwa kutoka Aleksanda wa Aleksandria)

Aleksanda I wa Aleksandria (alifariki tarehe 26 Februari[1] au 17 Aprili, 326 au 328) alikuwa Patriarki wa 19 wa Aleksandria, Misri, maarufu kwa imani na juhudi.

Picha takatifu katika monasteri Veljusa , Masedonia.

Wakati wa uongozi wake alikabili masuala mbalimbali, kama vile tarehe ya Pasaka, matendo ya Meletius wa Lycopolis, na hasa Uario. Ndiye aliyekuwa mpinzani mkuu wa padri Ario na wa mafundisho yake hadi Mtaguso wa kwanza wa Nisea, ambao aliushiriki uzeeni pamoja na maaskofu wengine 317 na ambao ulikataa uzushi huo hata kwa kutunga kanuni ya imani sahihi. Ndiye aliyemuandaa shemasi Atanasi wa Aleksandria kuwa mwandamizi wake.[2]

Tangu kale anaheshimiwa na Waorthodoksi wa Mashariki, Waorthodoksi na Wakatoliki kama mtakatifu[3].

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 26 Februari[4] au 29 Mei[5].

Maandishi hariri

Mengi kati ya maandishi yake hayakutufikia, isipokuwa barua mbili. Mengine hayana hakika.

Tazama pia hariri

Tanbihi hariri

Marejeo hariri

  • Alexander I (313–328). Official web site of the Greek Orthodox Patriarchate of Alexandria and All Africa. Iliwekwa mnamo 2011-02-08.

Viungo vya nje hariri

  Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.