Borno ni jimbo la Nigeria katika kaskazini ya nchi lenye wakazi milioni nne na nusu. Mji mkuu pia mji mkubwa wa jimbo ni Maiduguri (wakazi 1,112,511).

Wacheza ngoma, Borno
Ramani ya Borno

Imepakana na nchi jirani za Niger, Chadi na Kamerun, halafu majimbo ya Nigeria ya Adamawa, Yobe na Gombe.

Borno ni hasa eneo la Wakanuri. Jimbo la leo ni mabaki ya milki ya Bornu ya karne zilizopita. Milki hii ya Kanem-Bornu ilitawala eneo kubwa katika mazingira ya Ziwa Chadi kwa muda wa miaka 600 tangu mnamo 1300. Milki iliporomoka mwisho wa karne ya 19 na amiri yake ya mwisho aliuawa na Mwarabu Rabih az-Zubayr kutoka Sudan. Baada ya Wafaransa chini kumshinda Zubayr mwaka 1900 eneo la Bornu likagawiwa na nchi za Ulaya. Sehemu kubwa likawa chini ya Uingereza, na maeneo mengine chini ya Ufaransa na Ujerumani. Waingereza walirudishwa familia ya watawala wa Borno kwa cheo cha amiri wa Borno.

Katika Nigeria huru Bornu iliingizwa katika jimbo la Kaskazini-Mashariki lililogawiwa 1976. Jimbo kubwa la Borno likagawiwa tena kwa kutenga jimbo la Yobe.

Hadi leo amiri wa Borno ana athira kubwa katika siasa hata kama hana cheo cha kiserikali tena bali ya kiutamaduni tu.

Viungo vya Nje hariri


 
Majimbo ya Nigeria
 
Abia | Abuja Federal Capital Territory | Adamawa | Akwa Ibom | Anambra | Bauchi | Bayelsa | Benue | Borno | Cross River | Delta | Ebonyi | Edo | Ekiti | Enugu | Gombe | Imo | Jigawa | Kaduna | Kano | Katsina | Kebbi | Kogi | Kwara | Lagos | Nasarawa | Niger | Ogun | Ondo | Osun | Oyo | Plateau | Rivers | Sokoto | Taraba | Yobe | Zamfara
  Makala hii kuhusu maeneo ya Nigeria bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Borno (jimbo) kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.