Busagara ni kata ya Wilaya ya Kibondo katika Mkoa wa Kigoma, Tanzania.

Vijiji hariri

Busagara ni kata iliyopo katika tarafa ya Kifura. Kata ina vijiji 4: Kifura, Kigendeka, Kasaka na Nyaruyoba.

Historia hariri

Kabla ya kuanzishwa kwa vijiji vya ujamaa Busagara kilikuwa kijiji kilichokaliwa na Waha wa mdyank'o (kaya) wa Washubhi na ilikuwa moja kati ya himaya ya mwami Luhaga aliyeitawala Kibondo yote.

Baada ya uhuru mwaka 1961 wakazi walitakiwa kuishi katika vijiji vya ujamaa: ndipo walipoanzisha kijiji cha Kasanda ambacho kwa sasa kinajulikana kama Kifura; eneo ambao lililokuwa kijiji cha zamani cha Busagara kwa sasa ni mashamba.

Wakazi hariri

Katika sensa ya mwaka 2022 wakazi wa kata walihesabiwa kuwa 16,341 [1]. Wakati wa sensa iliyofanyika mwaka wa 2012, kata ilikuwa na wakazi wapatao 30,722 waishio humo.[2]

Uchumi hariri

Wakazi wa Busagara ni wakulima hasa wa mazao ya chakula kama vile mahindi, mihogo, maharage ya njano, mtama, karanga, magimbi n.k. Kilimo kinafanyika katika mashamba ya Kunk'ubha, Mrutunhu, Busagara, Mkugwa, Kihivfu nyensato n.k. Asilimia kubwa ya wakazi ni maskini.

Shule hariri

Kata ina shule za sekondari mbili: Moyowosi na Busagara.

Marejeo hariri

  Kata za Wilaya ya Kibondo - Mkoa wa Kigoma - Tanzania  

Bitare | Biturana | Bunyanbo | Busagara | Busunzu | Itaba | Kagezi | Kibondo Mjini | Kitahana | Kizazi | Kumsenga | Kumwambu | Mabamba | Misezero | Mukabuye | Murungu | Nyaruyoba | Rugongwe | Rusohoko

  Makala hii kuhusu maeneo ya Mkoa wa Kigoma bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Busagara kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.
Tafadhali usiingize majina ya maafisa au viongozi wa sasa maana wanabadilika mno.