Cristina Dorcioman

Cristina Dorcioman (alizaliwa 7 Agosti 1974) ni mwamuzi wa mpira wa miguu wa nchini Romania.

Mnamo 26 Julai 2013, Dorcioman alitangazwa kuwa mwamuzi wa michuano ya Fainali ya Euro ya UEFA ya Wanawake 2013 kati ya Ujerumani na Norwei kwenye Uwanja wa Friends Arena huko Solna, Uswidi .[1]

Pia alichezesha mechi ya nusu fainali ya kwanza kati ya Duisburg na Turbine Potsdam katika msimu wa 2010-11 wa Ligi ya Mabingwa ya UEFA, na robo fainali nyingine tatu za mashindano hayo. [2]

Mnamo 2009 alichezesha michuano ya UEFA Women's Euro na mwaka mmoja kabla alichezesha Fainali ya UEFA chini ya miaka 19 mwaka 2008 kati ya Italia na Norwei. [3]

Marejeo hariri

  1. "Dorcioman appointed to referee final". UEFA. 26 July 2013.  Check date values in: |date= (help)
  2. "Cristina Dorcioman". footballzz.co.uk. Iliwekwa mnamo 26 July 2013.  Check date values in: |accessdate= (help)
  3. "Cristina Dorcioman". WorldReferee.com. Ilihifadhi kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2016-08-22. Iliwekwa mnamo 26 July 2013.  Check date values in: |accessdate= (help)
  Makala hii kuhusu mtu huyo bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Cristina Dorcioman kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.