Daraja la Selander
Daraja la Selander ni daraja kwenye Barabara ya Ali Hassan Mwinyi (Bagamoyo Road) ambalo linavuka mto Msimbazi jijini Dar es Salaam, Tanzania.
Daraja la Selander English: Selander Bridge | |
---|---|
Yabeba | Barabara ya Ali Hassan Mwinyi (leni 4) |
Yavuka | Mkondo wa Msimbazi (Msimbazi Creek) |
Mahali | Oyster Bay, Dar es Salaam |
Mmiliki | Serikali ya Tanzania |
Urefu | mita 85 |
Kilifunguliwa | 1929 |
Anwani ya kijiografia | 6°47′46.69″S 39°16′52.81″E / 6.7963028°S 39.2813361°E |
Daraja hili lilitengenezwa mwaka 1929 likapewa jina kwa kumbukumbu ya John Einar Selander aliyekuwa mkurugenzi wa kwanza wa ujenzi katika eneo la Tanganyika chini ya utawala wa Waingereza.[1]
Daraja hili lilipanuliwa na Japan International Cooperation Agency mnamo 1980[2] kuwa na njia 4 za magari.
Tangu mwaka 2019 daraja la pili limeanza kujengwa takriban mita 300 kando yake upande wa Oyster Bay.
Marejeo hariri
- ↑ Brennan, James R.; Burton, Andrew; Lawi, Yusuf (2007). Dar es Salaam: Histories from an Emerging African Metropolis. Page 104, Mkuki na Nyota. Iliwekwa mnamo 7 March 2013. Check date values in:
|accessdate=
(help) - ↑ "30 Years Of JICA Tanzania Office (1980-2010)" (PDF). Page 6, Japan International Cooperation Agency. 2010. Ilihifadhi kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2016-03-04. Iliwekwa mnamo 7 March 2013. Check date values in:
|accessdate=
(help)
Makala hii kuhusu daraja barani Afrika bado ni mbegu. Unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuongezea habari. |