Fabian Delph

Wachezaji mpira wa Uingereza

Fabian Delph (alizaliwa 21 Novemba 1989) ni mchezaji wa soka wa Uingereza ambaye anacheza kama kiungo au beki wa kushoto wa klabu ya Manchester City FC na timu ya taifa ya Uingereza.

Delph akiwa Manchester City.

Alizaliwa huko Bradford, Delph alianza kazi yake ya soka katika chuo cha vijana cha Bradford City. Delph aliondoka Jijini mnamo Septemba 2001 na kwenda kujiunga na Leeds United baada ya kupendekezwa na kocha wao Greg Abbott.

Baada ya Leeds kushuka daraja, klabu kadhaa za Ligi Kuu ikiwa ni pamoja na Everton, Manchester City, Fulham, Sunderland, Tottenham Hotspur na Aston Villa walitaka saini ya Delph ili kumpata. Mnamo tarehe 3 Agosti 2009,Aston Villa walifanikiwa kuinasa saini ya Delph na kumsajili.

Tarehe 17 Julai 2015, Delph ilisaini mkataba wa miaka mitano na klabu ya Manchester City kwa ada ya £ milioni 8.

Makala hii kuhusu mchezaji mpira fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Fabian Delph kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.