Gdańsk (kwa Kijerumani: Danzig) ni mji wa bandari kaskazini mwa Poland kule ambako mto Vistula unaishia katika Bahari Baltiki.

Bendera ya mji.
Gdansk - Danzig : Mji wa Kale

Mji una wakazi wapatao 500,000 na bandari muhimu zaidi ya Poland.[1]

Historia hariri

Mji ukikuwepo tayari mnamo mwaka 900 BK na tangu mwaka 979 eneo lake liliingizwa mara ya kwanza katika milki ya Poland.

Katika karne ya 13 mtemi Swantopolk alikaribisha walowezi Wajerumani kuanzisha mji chini ya utaratibu wa kwao nyumbani. Mji huu wa Kijerumani ulikua na kuwa mji muhimu wa biashara na tasnifu ikaungana na makazi ya awali ya wazalendo.

Mji wa Danzig (jina la Kijerumani) uliendelea kuwa mji wa utamaduni wa Kijerumani lakini kwa karne kadhaa ulikuwa mji wa kujitawala chini ya Dola la Wamisalaba Wajerumani na baadaye chini ya mfalme wa Poland.

Baada ya magawio ya Poland ulikuwa mji wa Prussia tangu 1796 na baadaye mji wa Ujerumani.

Baada ya Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia Danzig ilitengwa na Ujerumani na kuwa Dola-mji hadi kuvamiwa na Ujerumani mwaka 1939. Mwisho wa Vita Kuu ya Pili ya Dunia mwaka 1945/1946 wakazi Wajerumani walifukuzwa na mji wote pamoja na maeneo ya mashariki mwa Ujerumani vilipata kuwa sehemu ya Jamhuri ya Poland. Sasa jina lake ni Gdansk.

Mji ulioharibika sana vitani ukajengwa upya kwa kuiga majengo ya awali. Katika miaka ya utawala wa kikomunisti katika Poland Gdansk iliendelea kuwa kitovu cha upinzani na mahali ambako chama cha Solidarnosc kilianzishwa.

Tanbihi hariri

  1. About Port. Port of Gdansk Authority. Iliwekwa mnamo 2009-11-05.