Hifadhi ya Taifa ya Ruvubu

Hifadhi ya Taifa ya Ruvubu, ni mbuga ya taifa nchini Burundi inayojumuisha kilomita za mraba 508, ambayo ilianzishwa mwaka 1980.

Mipaka yake iko ndani ya majimbo ya Karuzi, Muyinga, Cankuzo na Ruyigi . Hifadhi hii inagusa nchi jirani ya Tanzania upande wa kusini, bonde la Mto Ruvubu ambalo mandhari yake yametawala eneo hilo. 

Hifadhi ya Taifa ya Ruvubu imepata jina lake kutokana na Mto Ruvubu unaopita katika urefu wa hifadhi hiyo. [1] Hifadhi hii ni sehemu ya mwisho ya mfumo wa ikolojia wa nyasi asilia ambao hapo awali ulifunika sehemu kubwa ya kaskazini mashariki mwa Burundi.

Ni makazi kwa idadi ya spishi za wanyamapori, haswa kiboko, mamba wa Nile, nyati wa Cape, nyati, aina nyingi za duiker, spishi tano za nyani, ikiwa ni pamoja na nyani wa mzeituni, tumbili aina ya vervet, tumbili aina ya colobus, tumbili wa blue, na Senegal bushbaby . Takribani aina 200 za ndege zilirekodiwa katika mbuga hiyo. [1]

Marejeo hariri

  1. 1.0 1.1 INECN (1990). La Preservation de Notre Patrimoine Naturel. Les Presses Lavigerie, Bujumbura. 
  Makala hii kuhusu maeneo ya Afrika bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Hifadhi ya Taifa ya Ruvubu kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.