Kucha (Hyliota)

(Elekezwa kutoka Hyliotidae)
Kucha
Kucha mgongo-zambarau
Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Animalia (Wanyama)
Faila: Chordata (Wanyama wenye ugwe wa neva mgongoni)
Nusufaila: Vertebrata (Wanyama wenye uti wa mgongo)
Ngeli: Aves (Ndege)
Oda: Passeriformes (Ndege kama shomoro)
Familia ya juu: Passeroidea
Familia: Hyliotidae (Ndege walio na mnasaba na kucha (Hyliota))
Jenasi: Hyliota
Swainson, 1837
Ngazi za chini

Spishi 4:

Kucha wa jenasi Hyliota ni ndege wadogo ambao zamani waliainishwa katika Sylviidae, familia ya kucha wengine. Sasa wataalamu wanakubaliana kwamba ndege hawa hawana mnasaba na Sylviidae. Labda wana mnasaba na familia Promeropidae (ndegesukari wa Afrika Kusini). Hadhi yao haijaamua bado lakini wapewa familia yao kwa sasa: Hyliotidae. Wanafanana na tatata. Kucha hawa wana rangi ya nyeusi au zambarau mgongoni na nyeupe, machungwa au njano chini. Hula wadudu na pengine beri na mbegu. Hulijenga tago lao kwa umbo wa kikombe ndani ya uoto mzito. Jike huyataga mayai 2-5.

Spishi za Afrika hariri