Julita wa Kaisarea

Julita wa Kaisarea (alifariki Kaisarea wa Kapadokia, katika Uturuki ya leo, 303) alikuwa mfiadini wa Kikristo aliyechomwa moto kwa sababu alikataa katakata amri ya hakimu ya kutoa sadaka ya ubani kwa miungu.[1]

Anajulikana kupitia hotuba ya Bazili Mkuu katika siku ya kukumbuka kifodini chake.

Tangu kale anaheshimiwa na Wakatoliki na Waorthodoksi kama mtakatifu.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 30 Julai[2].

Tazama pia hariri

Tanbihi hariri

  Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.