Luigi Orione (Pontecurone, Piemonte, 23 Juni 1872Sanremo, Liguria, 12 Machi 1940) alikuwa padri wa Kanisa Katoliki kutoka Italia Kaskazini.

Sanamu ya Mt. Luigi Orione.

Alianzisha shirika la kitawa la Wana wa Maongozi ya Mungu limsaidie kukabili matatizo ya jamii hasa upande wa vijana.

Yote hayo yalitokana na huruma yake kubwa kwa maskini, ili kuwatimizia mahitaji yao duniani kote.

Alitangazwa na Papa Yohane Paulo II kwanza mwenye heri tarehe 26 Oktoba 1990, halafu mtakatifu tarehe 16 Mei 2004[1].

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe ya kifo chake[2].

Tazama pia hariri

Tanbihi hariri

Viungo vya nje hariri

 
Wikimedia Commons ina media kuhusu:
  Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.