Migdoni na wenzake

Migdoni na wenzake Eugeni, Masimo, Dominika, Mardoni, Smeraldi na Hilari (walifariki Nikomedia, leo Izmit nchini Uturuki, 303) walikuwa Wakristo wa mji huo ambao waliuawa wakati wa dhuluma ya kaisari Diokletian kwa sababu walikataa kuabudu miungu[1].

Walinyongwa mmoja kwa siku ili kuwatisha waliobaki. Migdoni alikuwa padri.

Wanaheshimiwa na Kanisa Katoliki, Waorthodoksi na Waorthodoksi wa Mashariki kama watakatifu wafiadini.

Sikukuu yao inaadhimishwa kila mwaka tarehe 12 Machi[2].

Tazama pia hariri

Tanbihi hariri

  Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.