Milima kunjamano (kwa Kiingereza fold mountains) ni aina ya milima ambayo hutokea wakati mabamba ya gandunia yanagongana. Shinikizo linasababisha kukunjwa kwa ganda la dunia na hili linafanya sehemu ya uso wa ardhi kuinuliwa juu.

Bamba la gandunia A linasukumwa chini ya bamba la gandunia B; shinikizo kwenye kona ya B inasababisha kupanda kwa milima kunjamano. Kona ya A inatelemka katika magma C ya koti ya dunia na kuyeyuka.
Mgongano wa mabamba mawili hujenga milima kunjamano
Safu sambamba za Rocky Mountains (Marekani)

Tokeo lake ni safu ya milima au pia mfululizo wa masafu yaliyo sambamba.

Milima kunjamano ni umbo la kawaida kati ya milima mirefu duniani. Mifano ni milima ya Atlas katika Afrika ya Kaskazini, Alpi katika Ulaya na Himalaya katika Asia. Kilimanjaro ni mlima mrefu kwa upande wa Afrika lakini si mlima kunjamano kwa sababu ni volkeno ya pekee.

Milima kunjamano muhimu

hariri

Afrika

hariri

New Zealand

hariri

Amerika ya Kaskazini

hariri

Amerika ya Kusini

hariri

Kujisomea

hariri
  Makala hii kuhusu mambo ya sayansi bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Milima kunjamano kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.