PI hariri

Kwa majina naitwa Innocent William Massawe, Nimezaliwa tarehe 12 Mei 1995, Nimesoma Shule ya St Jude kuanzia darasa la pili hadi kidato cha sita. kwa sasa ni mwanafunzi mwaka wa tatu Chuo kikuu cha Dar es Salaam masomo ya biashara (Bcom in Accounting)

Innocent and Magreth
rafiki kipenzi katika makutano ya pili ya wahitimu wa shule ya St Jude.
Jina la kuzaliwa Magreth, Innocent

ELIMU hariri

shule ya awali- Sikufanikiwa kusoma shule ya awali shule ya msingi- Shule ya msingi Kiserian Darasa la kwanza na la pili mwaka 2001 na 2002, The School of St Jude Darasa la pili hadi la saba mwaka 2003 hadi 2009 Shule ya Sekondari- The school of St Jude Kidato cha kwanza hadi kidato cha sita mwaka 2010 hadi 2016 ELimu ya juu- Chuo Kikuu cha Dar es Salaam mwaka 2017 hadi sasa

MAISHA hariri

Baada ya kumaliza Kisdato cha sita mwaka 2016, nilichaguliwa kuhudhuria mafunzo ya matendo na ukakamavu katika jeshi la kujenga taifa, kambi ya Mlale, Songea, Ruvuma, baada ya mafunzo nilifanya kazi ya jamii ambapo nilifundisha somo la hisabati katika shule ya sekondari Losirway, Moshono, Arusha kwa mda wa mwaka mmoja. Mwezi wa kumi 2017 nilijiunga na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kwa mafunzo ya elimu ya juu Maisha ya kawaida mimi napendelea michezo Michezo ninayoweza kucheza na niliyowah kushiriki kwenye mashindano ni pamoja na Mpira wa miguu, Mpira wa kikapu, Voliboli na Netiboli, Michezo niliyowahi kucheza kwa kujifurahisha ni Baseballl, Kriketi, Freesbee na riadha. Napenda pia kufuatilia michezo mbalimbali moja wapo ikiwa ni Langalanga. Ni mpenzi wa video games pia, nimeshacheza michezo kama need for speed, PES, FIFA, Assasin Creed, Just Cause, NBA live na Nyingine nyingi kutumia Simu. Mbali na michezo napenda pia muziki na filamu, Filamu nilizokwisha kuzitazama ni nyingi mno siwezi kuziorodhesha. mbali na vitu hivi mimi pia ni muandishi na mhariri wa makala ya Wikipedia.