Mzumai
Mizumai ikitoa mbegu (Chrysopogon zizanioides)
Mizumai ikitoa mbegu (Chrysopogon zizanioides)
Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Plantae (Mimea)
(bila tabaka): Angiospermae (Mimea inayotoa maua)
(bila tabaka): Monocots (Mimea ambayo mche wao una jani moja)
(bila tabaka): Commelinids (Mimea kama jaja)
Oda: Poales (Mimea kama manyasi)
Familia: Poaceae (Manyasi)
Nusufamilia: Andropogoneae
Jenasi: Chrysopogon
Spishi: C. zizanioides
(L.) Roberty

Mzumai (Chrysopogon zizanioides) au mkasikasi ni spishi ya nyasi katika nusufamilia Andropogoneae. Kwa asili spishi hii inatoka Uhindi lakini siku hizi hupandwa sana katika ukanda wa tropiki. Nchi kuu za uzalishaji ni Haiti, Uhindi, Java na Reunion.

Mzumai hupandwa sana kwa kuzuia mmomonyoko kwa sababu mizizi yake inapenya ardhi hadi m 3-4. Majani yanaweza kutumika kwa kulisha wanyama na kwa kutengeneza kamba, mikeka, vikapu n.k.. Mafuta yanasindikwa kutoka mizizi ambayo hutumika katika utamaradi, sabuni ya kiayurveda, dawa za ngozi na tendwa ya harufu.

Picha hariri