Nyamugali

Nyamugali ni kata ya Wilaya ya Buhigwe katika Mkoa wa Kigoma, mpakani mwa Tanzania na Burundi.

Wakati wa sensa iliyofanyika mwaka wa 2012, kata ilikuwa na wakazi wapatao 10,705 waishio humo.[1]

Kata hii imeundwa na vijiji viwili (Nyamugali na Burimanyi).

Hali ya hewa ya Nyamugali ni joto kiasi wakati wa masika (KIPINDI CHA MVUA) na baridi kiasi kwa kiangazi (hii hutokea pekee majira ya asubuhi na mchana jua huwa kali.

Shuguli za kiuchumi ni kilimo, usafirishaji, ufugaji, biashara pamoja na ufundi kama ushonaji wa nguo na unyoaji nywele. Kilimo kama shuguli kuu inayofanywa karibu na asilimia 90 ya wakazi wa Nyamugali bado sekta hii haijaendelea sana kwani vifaa duni ndizo nyezo zinazotumiwa.

Ugali wa mhogo ndio chakula kikuu kwa wakazi wa kata hii; vyakula vingine ni pamoja na viazi vitamu, maharage na ugali wa mahindi.

Elimu katika kata hii imekuwa ikiongozeka siku hadi siku huku ikikumbwa na uhaba wa shule za msingi na sekondari, shule ya sekondari Buha ikiwa ndiyo sekondari pekee inayohudumu kata hii pamoja na vijiji jirani vya Biharu na Kigege.

MarejeoEdit

  Kata za Wilaya ya Buhigwe - Mkoa wa Kigoma - Tanzania  

Biharu | Buhigwe | Bukuba | Janda | Kajana | Kibande | Kibwigwa | Kilelema | Kinazi | Mkatanga | Mubanga | Mugera | Muhinda | Munanila | Munyegera | Munzeze | Nyamugali | Muyama | Mwayaya | Rusaba