Porfiri wa Gaza (kwa Kigiriki Πορφύριος, Porphyrios; Thesalonike, Ugiriki[1]347 hivi – Gaza, Palestina, 26 Februari 420) alikuwa askofu wa mji huo kuanzia mwaka 395 hadi kifo chake.

Mchoro wa ukutani katika monasteri ya Dionisi huko Afon (Ugiriki).

Kutokana na masimulizi ya Maisha yake, yaliyoandikwa na Marko shemasi[2] alipata umaarufu kwa kuingiza katika Ukristo mji huo ulioshikilia bado Upagani na kwa kubomoa mahekalu yaliyokuweko, bila kujali dhuluma ndefu.

Kwanza alikuwa mmonaki miaka mitano huko Misri na mitano mingine ng’ambo ya mto Yordani, akijulikana kwa wema wake kwa watu fukara. [3].

Tangu kale anaheshimiwa na Wakatoliki, Waorthodoksi na Waorthodoksi wa Mashariki kama mtakatifu.

Sikukuu yake huadhimishwa katika tarehe ya kifo chake[4][1].

Tazama pia hariri

Tanbihi hariri

  1. 1.0 1.1 Great Synaxaristes: Ὁ Ἅγιος Πορφύριος Ἐπίσκοπος Γάζης. 26 Φεβρουαρίου. ΜΕΓΑΣ ΣΥΝΑΞΑΡΙΣΤΗΣ.
  2. Apparent use of Theodoret and other later sources convinced P. Peeters that it was actually written after 534. (P. Peeters, "La vie géorgienne de Saint Porphyre de Gaza" Analecta Bollandiana 59 1941, pp 65–216.
  3. Helen Saradi-Mendelovici, "Christian Attitudes toward Pagan Monuments in Late Antiquity and Their Legacy in Later Byzantine Centuries" Dumbarton Oaks Papers 44 (1990, pp. 47–61) pp 53f instances as history the destruction of the temples in Gaza in Vita Porphyrii.
  4. Martyrologium Romanum

Marejeo hariri

  • Thomas F. Head, Medieval Hagiography: an anthology, (Routledge) 2001.
  • Ramsay MacMullen, Christianizing the Roman Empire, (Yale University Press) 1984.

Viungo vya nje hariri

  Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.