Palestina (kwa Kiarabu: فلسطين‎ filasṭīn, falasṭīn; kutoka Kilatini: Palaestina; kwa Kiebrania: פלשתינה Palestina) ni jina la eneo lililoko upande wa Mashariki wa Bahari ya Mediteranea kati ya mkingo wa bahari hiyo na mto Yordani.

Palestina
Bendera
Nembo
Mji mkuu (na mkubwa zaidi){{{mji_mkuu}}}
{{{latd}}}°{{{latm}}}′ {{{latNS}}} {{{longd}}}°{{{longm}}}′ {{{longEW}}}
Lugha rasmi{{{lugha_rasmi}}}
Serikali{{{serikali}}}
{{{vyeo_viongozi}}}{{{majina_viongozi}}}
{{{muundo_uhuru}}}{{{tarehe_uhuru}}}
Eneo
 • Eneo la jumla{{{eneo_jumla}}}
 • Maji (%){{{maji}}}
Idadi ya watu
 • Kadirio la 2023{{{watu_kadirio}}}
Pato la TaifaKadirio la 2023
 • Jumla{{{pato}}}
 • Kwa kila mtu{{{pato_kwa_mtu}}}
Pato Halisi la TaifaKadirio la 2023
 • Jumla{{{pato_halisi}}}
 • Kwa kila mtu{{{pato_halisi_kwa_mtu}}}
Maendeleo ({{{mwaka_maendeleo}}}){{{maendeleo}}}
Fedha{{{fedha}}}
Majira ya saa{{{majira_saa}}}
Muundo wa tareheDD/MM/YYYY
Ramani ya maeneo yanayotazamiwa kuwa chini ya Mamlaka ya Kitaifa ya Palestina
Yerusalemu kutoka Mlima wa Mizeituni
Palestina 1759
Palestina 1851
Palestina 1864
Palestina 1900
Palestina 1915
Palestine 1920
Palestina 1924
Palestina 1946
Palestina 1947

Historia ya jina na eneo la Palestina hadi 1948

Asili ya jina ilikuwa nchi ya Wafilisti iliyokuwa kanda nyembamba ya ardhi karibu na pwani ya bahari. Waroma wa kale walitumia jina hilo kwa jumla ya jimbo lao katika sehemu hizi.

Baada ya uvamizi wa Waarabu Waislamu jina liliendelea kutumiwa kwa umbo la Kiarabu "Filastin" na kutazamwa kama sehemu ya Shamu au Syria.

Tangu mwaka 1516 eneo lilitawaliwa na Milki ya Osmani. Kwa muda mrefu maeneo ya Palestina yalikuwa sehemu ya kusini ya jimbo la Dameski, na katika karne ya 19 jimbo la pekee la Yerusalemu liliundwa.

Baada ya Vita Kuu ya Kwanza ya Dunia Uingereza ulitawala eneo hili kama eneo la kukabidhiwa la Shirikisho la Mataifa, na eneo hili lilikuwa pamoja na sehemu kubwa upande wa mashariki wa mto Yordani. Waingereza waligawa eneo katika sehemu mbili upande wa magharibi (Palestina yenyewe) na upande wa mashariki wa mto Yordani uliokuwa baadaye milki ya Yordani.

Kwenye sehemu ya magharibi iliyokuwa Palestina yenyewe kulikuwa na uhamiaji wa Wayahudi kutoka nchi za Ulaya ulioweka msingi kwa mapambano kati ya Israeli na Palestina ya baadaye.

Mwaka 1947 Umoja wa Mataifa uliamua kugawa Palestina katika sehemu tatu zilizopangwa kama Dola la Kiyahudi, Dola la Kiarabu na Yerusalemu kama mji wa kimataifa. Lakini Wayahudi walitangaza uhuru wa Dola la Israeli. Wenyeji Waarabu walipinga azimio hili na vita ilitokea. Baada ya mkataba wa kusalimisha amri Israeli mpya ilikuwa na sehemu ya Palestina kubwa kuliko awali. Asilimia kubwa ya wakazi Waarabu wa sehemu zilizokuwa chini ya Israeli mpya walikimbia au walifukuzwa nje. Ukanda wa Gaza ulishikwa na Misri na Ukingo wa Magharibi wa Yordani ulitawaliwa na milki ya Yordani.

Mapigano ya Wapalestina

Kati ya wakimbizi Waarabu waliokaa katika makambi huko Lebanoni, Syria, Yordani na Gaza kulikuwa na harakati ya kujielewa kama taifa la Wapalestina wakaunda vyama mbalimbali vya kupigania kurudi kwao lakini hii ilishindikana. Baada ya Vita ya siku 6 mwaka 1967 Gaza na Ukingo wa Magharibi wa Yordani zilitwaliwa na jeshi la Israeli.

Harakati ya Wapalestina Waarabu iliendelea kupigania uhuru. Mapigano haya yalipata namna ya usuluhisho kwa muda na katika mapatano ya Oslo mwaka 1993 yalianzishwa Mamlaka ya Kitaifa ya Palestina yaliyotangaza Dola la Palestina.

Palestina mpya

Kwa sasa Palestina ni nchi katika mwendo wa kupata uhuru kamili lakini hakuna uhakika mwendo huu utakamilishwa lini.

Maeneo ya Palestina yanatengwa kati ya sehemu chini ya serikali ya Palestina na maeneo yanayosimamiwa na Israeli.

Maeneo haya yako kati ya mto Yordani na pwani ya Mediteranea: ni hasa Ukingo wa Magharibi wa Yordani na Ukanda wa Gaza.

Mamlaka ya Kitaifa ya Palestina ina kiwango fulani cha madaraka ya kiserikali katika baadhi ya maeneo haya.

Mamlaka hayo hutambuliwa na nchi nyingi za Waarabu kama serikali halisi. Jumuia ya kimataifa kwa ujumla imetambua mamlaka kwa viwango mbalimbali lakini si kama serikali kamili ya nchi huru. Hivyo Mamlaka ina kiti cha mtazamaji kwenye Umoja wa Mataifa.

Maeneo ya Palestina ya sasa yamepakana na Israel, Yordani na Misri. Kanda la Gaza lina pwani kwenye Mediteranea.

Ramani za mabadiliko ya mipaka ya Palestina

Tazama pia

Viungo vya nje

Serikali

Israeli na Mamlaka ya Palestina

Nchi na maeneo ya Asia

Afghanistan | Armenia2 | Azerbaijan | Bahrain | Bangladesh | Bhutan | Brunei | China | Falme za Kiarabu | Georgia2 | Hong Kong3 | Indonesia | Iraq | Israel | Jamhuri ya China (Taiwan) | Japani | Kamboja | Kazakhstan | Kirgizia | Korea Kaskazini | Korea Kusini | Kupro2 | Kuwait | Laos | Lebanoni | Macau3 | Malaysia | Maldivi | Mongolia | Myanmar | Nepal | Omani | Pakistan | Palestina | Qatar | Saudia | Singapuri | Sri Lanka | Syria | Tajikistan | Timor ya Mashariki | Turkmenistan | Uajemi | Ufilipino | Uhindi | Urusi1 | Uthai | Uturuki1 | Uzbekistan | Vietnam | Yemen | Yordani

1. Nchi ina maeneo katika Asia na Ulaya. 2. Nchi iko Asia lakini inahesabiwa pia kati ya nchi za Ulaya kwa sababu za historia au utamaduni. 3. Eneo la pekee la China.


  Makala hii kuhusu maeneo ya Asia bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Palestina kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.