Ruaruke ni kata ya Wilaya ya Kibiti katika Mkoa wa Pwani, Tanzania, yenye postikodi namba 61812.

Katika sensa ya mwaka 2022 wakazi walihesabiwa 11,283 [1]. Wakati wa sensa iliyofanyika mwaka wa 2012, kata ilikuwa na wakazi wapatao 7,229 [2] walioishi humo.

Wakazi ni hasa Wandengereko na Wamyagatwa (Wazaramo) pia kuna makabila mengine ya wahamiaji kama vile Wasukuma, Wamang'ati na Waha.

Dini kuu ni Uislamu na Ukristo.

Wakazi wa Ruaruke wanajishughulisha zaidi na kilimo pamoja na ufugaji wa kuku wa kienyeji. Mazao yanayolimwa ni ya biashara na chakula. Mazao ya biashara ni korosho, ufuta na mihogo. Mazao ya chakula ni mpunga na mahindi; mihogo hutumika kama zao la chakula na la biashara.

Marejeo hariri

  1. https://www.nbs.go.tz/
  2. "Sensa ya 2012, Pwani - Rufiji DC". Ilihifadhi kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2016-03-03. Iliwekwa mnamo 2016-06-18. 
  Kata za Wilaya ya Kibiti - Mkoa wa Pwani - Tanzania
 

Bungu | Dimani | Kibiti | Kiongoroni | Mahege | Maparoni | Mbuchi | Mchukwi | Mjawa | Mlanzi | Msala | Mtawanya | Mtunda | Mwambao | Ruaruke | Salale


  Makala hii kuhusu maeneo ya Mkoa wa Pwani bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Ruaruke kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.
Tafadhali usiingize majina ya maafisa au viongozi wa sasa maana wanabadilika mno.