Stefano Harding (Sherborne, Dorset, Uingereza, 1060 hivi - Citeaux, Ufaransa, 28 Machi 1134) alikuwa mmonaki[1], padri, mwanzilishi mmojawapo[2] na abati[3] wa urekebisho wa Citeaux wa shirika la Benedikto wa Nursia.

Mchoro wa ukutani wa Mt. Stefano Harding.
Mchoro wa ukutani wa Mt. Stefano Harding.

Alifika Cîteaux kutoka Molesme pamoja na wamonaki wengine, akaongoza monasteri hiyo na kuanzisha huko tabaka la mabradha.

Katika uongozi wake wa miaka 25 aliongeza monasteri 12 alizoziunganisha chini ya Mwandiko wa Upendo, ili kusiwe na ugomvi wowote kati ya wamonaki bali wote waishi kwa kufuata amri ya upendo, kanuni moja na desturi za kufanana. Ndiye aliyempokea utawani Bernardo wa Clairvaux na wenzake 30[4][5].

Tangu kale anaheshimiwa kama mtakatifu.

Sikukuu yake inaadhimishwa kila mwaka tarehe 28 Machi[6].

Tazama pia hariri

Tanbihi hariri

  1. "The Sherborne Register 1550-1950". Old Shirbirnian Society. Iliwekwa mnamo 8 February 2019.  Check date values in: |accessdate= (help)
  2. Hollingsworth, Gerelyn. "St. Stephen Harding", National Catholic Reporter, March 28, 2011
  3. "ST. STEPHEN HARDING :: Catholic News Agency (CNA)", Catholic News Agency. Retrieved on 2021-03-24. (en) Archived from the original on 2017-04-19. 
  4. Huddleston, Gilbert. "St. Stephen Harding." The Catholic Encyclopedia Vol. 14. New York: Robert Appleton Company, 1912.
  5. http://www.santiebeati.it/dettaglio/49800
  6. Martyrologium Romanum

Marejeo hariri

  • Claudio Stercal, Stephen Harding: A Biographical Sketch and Texts (Trappist, Kentucky: Cistercian Publications, 2008) (Cistercian Studies Series, 226).

Viungo vya nje hariri

 
Wikimedia Commons ina media kuhusu:
  Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.