Theluji (kutoka Kiarabu ثلج, thalj) ni aina ya pekee ya barafu ya maji. Inapatikana kama usimbishaji unaotelemka kwa maumbile ya barafu ya fuwelia. Fuwele za theluji ni ndogo; muundo wa fuwele unaonekana kwa macho matupu kama fuwele ni kubwa. Vipande vyake ni vyembamba sana, hivyo theluji hutelemka nyepesi si kama vipande vizito vya mvua ya mawe.

Maumbile ya fuweli za theluji
Nchi iliyofunikwa na theluji
Mazingira ya theluji huko Lapland, sehemu ya kaskazini ya Ufini
Mimea inayotokea wakati wa theluji kuyeyuka

Theluji haipatikani kwa halijoto juu ya 0 . Katika Afrika inaweza kutokea tu kwenye milima mirefu kama mlima Kilimanjaro na Mlima Kenya.

Asili ya Theluji hariri

Theluji hutokea kama mvuke wa maji mawinguni unafikia halijoto chini ya -10 C°. Maji mawinguni yanaweza kukaa kiowevu (majimaji) hata chini ya 0 C° kwa muda. Matone yake madogo sana yanaanza kushikana na punje ndogo za vumbi hewani na kuganda. Fuweli ndogo (chini ya mm 0,1) hutokea. Kadiri zinavyokua na kuwa nzito zinaanza kushuka. Njiani mvuke baridi inashikana na fuweli zinazoendelea kukua. Maumbile yanatokea ya kufanana na picha ya nyota.

Aina za theluji hariri

Watu katika nchi baridi wamezoea kutofautisha aina mbalimbali za theluji. Lugha nyingi zina maneno ya pekee kwa ajili ya aina tofauti za theluji, kama ni nyepesi au nzito, chepechepe au kavu, mpya au kama imeshakaa muda fulani.

Theluji inatokea:

  • kavu na nyepesi au bichi na nzito
  • kama mchanganyiko wa theluji na mvua ikiwa theluji imeanza kuyeyuka wakati wa kunyesha kutokana na kupitia kanda la hewa isiyo baridi
  • kufunikwa na ganda la barafu kama imeshakaa chini kwa siku kadhaa na jua liliwaka na kuyeyusha theluji ya juu kidogo. Theluji hii inaganda tena na kuwa barafu juu ya theluji ya chini.

Picha hariri