Umisionari ni utendaji unaolenga kueneza dini fulani, hasa zile zinazokusudiwa kuwa za kimataifa kutokana na misingi ya imani yake, kwamba ndivyo Mungu anavyotaka na alivyoagiza.

Asili ya neno hilo ni missio (kwa Kilatini utume).

Mmisionari au mwanamisheni ndiye mtu anayefanya kazi hiyo, hasa katika maeneo ambayo dini hiyo haipo au haijakua.

Mara nyingi wamisionari wanachangia pia maendeleo ya jamii, hasa kupitia elimu, utabibu, utunzaji wa watoto yatima na walioathiriwa na vita na maradhi mbalimbali.

Pengine uenezaji wa dini unatumia mbinu zisizokubalika kijamii, kama vile kulazimisha kwa namna moja au nyingine mtu asiyetumwa na moyo wake kukubali dini mpya.

Viungo vya nje hariri

 
Simple English Wiktionary
Wikamusi ya Kiswahili ina maelezo na tafsiri ya maana ya neno:
  Makala hii kuhusu mambo ya dini bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu mada hii kama historia yake au uenezi wake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.