Vikta Mwafrika (kwa Kilatini: Victor Maurus) alikuwa askari Mkristo kutoka Mauretania (katika Algeria ya leo).

Mozaiki katika kanisa lake mjini Milano.

Mwaka 303 BK, akiwa Milano (nchini Italia), alibomoa altare kadhaa za dini za jadi za Dola la Roma.

Kwa sababu hiyo aliteswa mbele ya Kaizari Maximian na hatimaye kuuawa pamoja na Waberberi wenzake Nabore na Feliche tarehe 12 Julai huko Lodi (Lombardia)[1].

Tangu kale anaheshimiwa na Wakatoliki, Waorthodoksi na wengineo kama mtakatifu mfiadini.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 8 Mei[2].

Tazama pia hariri

Tanbihi hariri

  1. https://www.santiebeati.it/dettaglio/62000
  2. Martyrologium Romanum: ex Decreto Sacrosancti oecumenici Concilii Vaticani II instauratum auctoritate Ioannis Pauli P.P. II promulgatum, Romae 2001, ISBN 8820972107

Viungo vya nje hariri

 
Wikimedia Commons ina media kuhusu:
  Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.