Andrianampoinimerina

Andrianampoinimerina (1787-1810) alikuwa muasisi wa ufalme wa Merina (Madagaska) ambaye alipata madaraka yake na kuimarisha nafasi yake katika uwanda wa juu wa kati wa kisiwa cha Madagaska katika karne ya 19.

Mchoro wa mwaka 1905 wa Ramanankirahina ukionyesha Andrianampoinimerina alivyoweza kuwa.

Mwaka 1875, Andrianampoinimerina alijipa madaraka ya kuwa mfalme wa mojawapo ya falme zilizokuwa zikipigana vita katika Imerina ya kati baada ya kumpindua mtawala aliyepita.

Kwa kutumia mbinu za kidiplomasia na za kijeshi aliendelea kuzichukua tawala za jirani katika himaya yake.

Mnamo mwaka 1792 aliuhamishia mji mkuu wake huko Antananarivo, ambapo alianza kujenga mifumo ya kisiasa na ya kijamaa ya ufalme mpya.

Baada ya mwaka 1800 alianzisha sera ya kuyapiga vita majimbo mengine visiwani humo kwa nia ya kuyaunganisha makabila yote 18.

Katika kutimiza jukumu hilo, alikabiliana na upinzani wa hali ya juu kutoka kwa makabila mengine kisiwani humo kama vile Wasakalava, Wabezanozano na Waambongo.

Hata hivyo, wakati wa kifo chake hapo 1810, Andrianampoinimerina alikuwa ameifanya tayari Imerina kuwa pengine ufalme wenye nguvu zaidi kuliko falme zote katika kisiwa cha Bukini.

Makala hii kuhusu mwanasiasa fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Andrianampoinimerina kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.