Aureus wa Mainz (alifariki 451 hivi) alikuwa askofu wa kwanza kujulikana wa Mainz, leo nchini Ujerumani, katika nusu ya kwanza ya karne ya 5, akitokea Ufaransa ya leo.

Mt. Aureus, Heilbad Heiligenstadt.

Alidhulumiwa kwa kutetea imani sahihi ya Kanisa Katoliki dhidi ya Waario na hatimaye aliuawa na wavamizi Wahunni Wapagani wakati wa kuadhimisha Misa[1].

Anaheshimiwa kama mtakatifu mfiadini pamoja na dada yake Yustina na wenzao.

Sikukuu yao huadhimishwa tarehe 16 Juni[2].

Tazama pia hariri

Tanbihi hariri

Marejeo hariri

  • (Kijerumani) Hans Werner Nopper: Die vorbonifatianischen Mainzer Bischöfe, Books on Demand, Norderstedt 2001.

Viungo vya nje hariri

  Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.