Bartolomea Capitanio

Bartolomea Capitanio (13 Januari 1807 - 26 Julai 1833) alikuwa mwanamke bikira wa Italia kaskazini ambaye, pamoja na Visensya Gerosa, alianzisha shirika la Masista wa Upendo wa Lovere, ambao kwa kawaida wanaitwa Masista wa Maria Mtoto.

Maisha hariri

Bartolomea alizaliwa katika kijiji cha Lovere, mkoani Lombardia.

Alipokutana na Visensya waliungana kupambana na ujinga na ufukara wa watu wa eneo lao.

Mwaka 1833 walisaini hati ya kuanzisha shirika, ila baada ya miezi tu alifariki kwa ugonjwa wa kifua kikuu lakini hasa kwa kuunguzwa na upendo[1].

Hata hivyo Visensya aliendeleza shirika lao kwa miaka mingi akafariki mwaka 1847 hukohuko Lovere.

Wote wawili walitangazwa wenye heri na Papa Pius XI tarehe 30 Mei 1926, halafu watakatifu na Papa Pius XII tarehe 18 Mei 1950.

Sikukuu ya Bartolomea inaadhimishwa kila mwaka tarehe 26 Julai[2].

Tazama pia hariri

Tanbihi hariri

Marejeo hariri

  • Attwater, Donald; Catherine Rachel John (1993). The Penguin Dictionary of Saints (3rd ed.). New York: Penguin Books. ISBN 0140513124. 
  • G. Lubich, P. Lazzarin, Bartolomea Capitanio, una possibile compagna di viaggio, Città Nuova, 1982

Viungo vya nje hariri

 
WikiMedia Commons
  Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.