Bizanti (pia Byzantium au Byzantion kutoka kwa Kigiriki Βυζάντιον) ilikuwa mji wa Ugiriki ya Kale. Wakati wa Dola la Roma jina lake lilibadilishwa kuwa Konstantinopoli na tangu karne ya 20 inajulikana kama Istanbul.

Mahali pa Bizanti (Konstantinopoli, Istanbul)
Rasi ya Bizanti

Jina hariri

Jina la Kigiriki Byzantion liliendelea kutumika kama jina badala ya Konstantinopoli mara kwa mara na kuwa chanzo cha "Ufalme wa Bizanti" jinsi sehemu ya mashariki ya Dola la Roma ilivyoitwa baada ya mwisho wa utawala wa Kiroma katika magharibi. [1] [2]

Historia hariri

Mji wa Bizanti uliundwa na Wagiriki kutoka Megara katika karne ya 7 KK ukaendelea kuwa mji wenye lugha ya Kigiriki hadi uvamizi wake na Milki ya Osmani mnamo 1453 BK. [3] Mji uliundwa kwenye rasi iliyopo baina ya Bahari ya Marmara na mkono wa bahari inayojulikana kama "Pembe ya Dhahabu" hivyo inazungukwa na maji kwa pande tatu iliyosaidia kutetea mji.

Hakuna uhakika kuhusu vyanzo vya Bizanti. Kufuatana na kisa kimoja mji ulianziswa na Byzas, mwana wa mfalme wa Megara iliyokuwepo karibu na Athene. Herodoti alitaja mwaka 667 KK kama mwaka wa kuundwa kwa mji, hivyo miaka 17 baada ya mji wa Kalsedonia uliopo upande mwingine wa mlangobahari wa Bosporus. [4]

Bizanti ilikuwa hasa mji wa biashara kutokana na mahali pake kwenye lango pekee la Bahari Nyeusi. Bizanti baadaye ilivamia Kalsedonia iliyopo kuvukia Bosporus upande wa Asia iliyoendelea kama sehemu ya Bizanti.

Katika karne ya 4 BK, wakati ilipokuwa sehemu ya Dola la Roma, Bizanti iliteuliwa na Kaizari Konstantino I kama mji wake mkuu ikajulikana pia kama "Nova Roma" (Roma Mpya) akiipamba na majengo mengi mazuri. Baadaye jiji hilo liliitwa Konstantinopoli (Kigiriki Κωνσταντινούπολις, Konstantinoupolis, yaani "mji wa Konstantino").

Marejeo hariri

  1. Speake, Jennifer, ed. (2003). Literature of Travel and Exploration: A to F. p. 160. ISBN 9781579584252. 
  2. Kazhdan, A. P.; Epstein, Ann Wharton (February 1990). Change in Byzantine Culture in the Eleventh and Twelfth Centuries. University of California Press. p. 1. ISBN 9780520069626. Byzantion term remained used for Constantinople. 
  3. The Rise of the Greeks. Orion Publishing Group. 2012. p. 22. ISBN 978-1780222752. 
  4. Ramsköld, Lars (2018). "The silver emissions of Constantine I from Constantinopolis, and the celebration of the millennium of Byzantion in 333/334 CE". Jahrbuch für Numismatik und Geldgeschichte 68: 145–198. 

Viungo vya nje hariri