Bujugo ni jina la kata ya Wilaya ya Bukoba Vijijini katika Mkoa wa Kagera, Tanzania yenye postikodi namba 35207 [1]. Wakati wa sensa iliyofanyika mwaka wa 2012, kata ilikuwa na wakazi wapatao 7,140 waishio humo.[2]

Wakazi wengi wa Bujugo ni Wahaya.

Kata ya Bujugo ni muungano wa vijiji vitatu ambavyo ni: Katoju, Buganguzi na Minazi. Kata ya Bujugo ina shule ya sekondari moja ambayo ni Bujugo sekondari. Bujugo ina shule za msingi nne ambazo: ni Bujugo, Minazi, Lutimbiro na Katoju.

Makao makuu ya kijiji cha Bujugo yako katika kitongoji cha Bituntu anakotokea Charles Delfinus Mtajwaha.

Shughuli za kiuchumi ni kilimo cha mazao ya chakula kama ndizi, mihogo, viazi, mahindi, maharagwe, karanga, njugu mawe n.k. Pia kuna mazao ya biashara kama kahawa, ndizi, majani ya chai na upandaji miti hasa ya mbao.

Marejeo hariri

  1. Nakala iliyohifadhiwa. Jalada kutoka ya awali juu ya 2018-08-05. Iliwekwa mnamo 2018-02-01.
  2. Sensa ya 2012, Kagera - Bukoba-District-Council
  Kata za Wilaya ya Bukoba Vijijini - Mkoa wa Kagera - Tanzania
 

Behendangabo | Bujugo | Butelankuzi | Ibwera | Izimbya | Kaagya | Kaibanja | Kanyangereko | Karabagaine | Kasharu | Katerero | Katoma | Katoro | Kemondo | Kibirizi | Kikomelo | Kishanje | Kishogo | Kyaitoke | Kyamulaile | Maruku | Mikoni | Mugajwale | Nyakato | Nyakibimbili | Rubafu | Rubale | Ruhunga | Rukoma


  Makala hii kuhusu maeneo ya Mkoa wa Kagera bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Bujugo kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.
Tafadhali usiingize majina ya maafisa au viongozi wa sasa maana wanabadilika mno.