Mkoa wa Kagera
Mkoa wa Kagera kati ya mikoa 31 ya Tanzania ndio mkoa wa kaskazini-magharibi kabisa. Unapakana na Burundi, Rwanda na Uganda upande wa Magharibi na Kaskazini. Upande wa Kusini na Mashariki umepakana na mikoa mingine ya Tanzania, yaani mkoa wa Kigoma na mkoa wa Geita. Eneo lake ni km² 28,953 za nchi kavu na km² 11,885 za maji ya ndani, hasa ya Viktoria Nyanza, jumla km² 40,838. Jina lake linatokana na mto Kagera unaouzunguka. Sensa ya mwaka 2022 imeonyesha idadi ya wakazi kuwa 2,989,299 inayoendelea kuongezeka kasi [1]. Makao makuu ya mkoa ni mji wa Bukoba.
Mkoa wa Kagera |
|
![]() |
|
Majiranukta: 1°55′S 31°18′E / 1.917°S 31.300°E | |
Nchi | Tanzania |
---|---|
Wilaya | 8 |
Mji mkuu | Bukoba |
Serikali | |
- Mkuu wa Mkoa | Meja General Marco Gatitu |
Eneo | |
- Jumla | 40,838 km² |
- Kavu | 28,953 km² |
- Maji | 11,885 km² |
Idadi ya wakazi (2022) | |
- Wakazi kwa ujumla | 2,989,299 |
Tovuti: http://www.kagera.go.tz/ |

Kiutawala eneo la mkoa limegawiwa kwa wilaya nane: Bukoba, Misenyi, Muleba, Karagwe, Ngara, Biharamulo na Kyerwa pamoja na manisipaa ya Bukoba. Misenyi ni wilaya mpya iliyoanzishwa mwaka 2007 na Kyerwa ikafuata mwaka 2012.
Mkoa huu una makabila makubwa manne ambayo ni Wahaya, Wanyambo, Wahangaza na Washubi. Wahaya huishi kwa wingi katika wilaya za Bukoba, Muleba na Misenyi, Wanyambo huishi kwa wingi katika wilaya za Kyerwa na Karagwe, Wahangaza huishi kwa wingi katika wilaya ya Ngara, na Washubi huishi kwa wingi katika wilaya ya Biharamulo. Makabila ya Wanyambo na Wahaya hupenda kula ndizi kwa wingi na asilimia kubwa wanafuata mila na desturi za mababu: zamani Wanyambo na Wahaya walikuwa hawawezi kuoana na hiyo bado sasa ipo kwa kiasi kidogo.
Pia mkoa huo una wakimbizi wengi, kwa asilimia kubwa wanatokea nchi za Rwanda na Burundi wakipitia wilaya ya Ngara.
Jiografia
haririMkoa wa Kagera uko mnamo mita 1000 juu ya uwiano wa bahari. Hali ya hewa ni nzuri kwa kuishi, kilimo, uvuvi. Mkoa huo ni maarufu kwa ulimaji wa kahawa, ndizi, miwa na chai.
Pia una mbuga 3 za wanyama: hifadhi ya Burigi-Chato, hifadhi ya Ibanda-Kyerwa, hifadhi ya Rumanyika-Karagwe.
Historia ya mkoa
haririMkoa huu unapatikana ukanda wa ziwa Viktoria. Katika mkoa huu kuna mambo mengi ambayo yalitetemesha nchi ya Tanzania. Mambo hayo ni pamoja na vita ya Uganda na Tanzania, vita ambavyo vilihusishwa na mkoa huu; ilikuwa mwaka 1978.
Ndipo Idd Amin Dada aliyekuwa Rais wa Uganda alipoliamru jeshi lake kuvamia mkoa wa Kagera. Walianza kuvamia wilaya ya Missenyi. Hapo Julius K. Nyerere aliyekuwa rais wa Tanzania aliamuru jeshi lake kufukuza wavamizi hadi kuvamia nchi ya Uganda.
Agizo hilo lilikuwa zuri lakini vijana wa mkoa wa Kagera walipata shida kwa sababu walilazimishwa kufuzwa Uanamgambo mara moja na kupelekwa vitani. Walipoanza tu vita hivyo raia wa Uganda walishirikiana na jeshi la Tanzania kufichua maficho ya jeshi la Uganda. Jeshi la Tanzania liliwapiga na kuwapora mali zao, vifaa vya kivita na kuwateka wanajeshi wao.
Mwanzoni mwa mwaka wa 1979 Idd Amin Dada alikimbia na Tanzania kushinda vita hivyo. Mara baada ya vita hivyo Watanzania walichukua mali za Uganda, hasa mifugo, na walipofika nchini Tanzania walifurahia na kusherekea ushindi huo.
Mwaka 1996 meli ya MV Bukoba ilizama ikisafirisha abiria kutoka mkoa wa Kagera kwenda Mwanza; watu wengi walikufa na lilikuwa pigo kwa serikali, kwa ndugu na majonzi makubwa kwa Watanzania kwa ujumla. meli hiyo ilikuwa ina mkoani mwanza katika ziwa la victoria
Katika mkoa huohuo mwaka 2016 lilitokea tetemeko la ardhi lililoleta maafa makubwa: watu walikufa, wengine walipoteza mali zao, hususani majumba yao. Uongozi wa mkoa wa Kagera uliomba kila Mtanzania kuchangia angalau shilingi 100 na kuwasaidia.
Elimu
haririKatika mkoa huu elimu bado imeenea sehemu nyingi na ni mkoa wenye wasomi wengi ingawa kuna baadhi ya watu walioko vijijini elimu haijawafikia vya kutosha. Elimu inakua kwa kasi ya wastani watu wengi wa mkoa huu ni wasomi, wengi wanafanya kazi ya kulima na biashara.
Majimbo ya bunge
haririWakati wa uchaguzi mkuu wa Tanzania mwaka 2015 mkoa huu ulikuwa na majimbo ya uchaguzi yafuatayo:
- Biharamulo : mbunge ni Oscar Rwegasira Mukasa (CCM)
- Bukoba Mjini : mbunge ni Steven L. Byabato (CCM)
- Bukoba Vijijini : mbunge ni Rweikiza Jasson (CCM)
- Karagwe : mbunge ni Innocent Luugha Bashungwa (CCM)
- Kyerwa : mbunge ni Innocent Sebba Balikwate (CCM)
- Muleba Kaskazini : mbunge ni Charles Mwijage ((CCM)
- Muleba Kusini : mbunge ni (CCM)
- Ngara : mbunge ni Alex Gashaza (CCM)
- Nkenge : mbunge ni Diodorius Kamala (CCM)
Tazama pia
haririTanbihi
haririViungo vya nje
hariri- Tovuti ya Mkoa wa Kagera (Kiswahili)
- Kagera – Bukoba – the official webguide Ilihifadhiwa 11 Aprili 2005 kwenye Wayback Machine. (Kiingereza)
- – Tourist Office Bukoba / Kagera (Kiingereza)
- United Republic of Tanzania: Kagera Region (Kiingereza)
- Utamaduni wa Kagera [http://web.archive.org/20051221194701/http://www.kagera.org/culture/index.htm Ilihifadhiwa 21 Desemba 2005 kwenye Wayback Machine. (Kiingereza)
Arusha | Dar es Salaam | Dodoma | Geita | Iringa | Kagera | Katavi | Kigoma | Kilimanjaro | Lindi | Manyara | Mara | Mbeya | Morogoro | Mtwara | Mwanza | Njombe | Pemba Kaskazini | Pemba Kusini | Pwani | Rukwa | Ruvuma | Shinyanga | Simiyu | Singida | Songwe | Tabora | Tanga | Unguja Kaskazini | Unguja Kusini | Unguja Mjini Magharibi |
Makala hii kuhusu maeneo ya Mkoa wa Kagera bado ni mbegu. Je unajua kitu kuhusu Mkoa wa Kagera kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni? Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa? Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari. Tafadhali usiingize majina ya maafisa au viongozi wa sasa maana wanabadilika mno. |