Kaliforni

(Elekezwa kutoka Californium)

Kaliforni (Californium) ni elementi ya kikemia yenye alama Cf na namba atomia 98. Ni metali nururifu iliyopangwa katika kundi la aktinidi kwenye jedwali la elementi. Isotopi kadhaa huwa na nusumaisha ya miaka mamia hadi 13,000 lakini isotopi nyingi hudumu dakika chache tu. [1]

Kaliforni haipatikani kiasili, ni elementi sintetiki. Ilitengenezwa mara ya kwanza kwenye mwaka 1950 na wanasayansi katika maabara ya Chuo Kikuu cha Kalifornia mjini Berkeley na kupokea jina la jimbo hilo. Ilipatikana baada ya kufyatulia chembe alfa kwa atomi za Curi.

Kaliforni ni kati ya elementi sintetiki chache zinazotumiwa lakini kwa tahadhari kubwa kwa sababu ya unururifu wake ulio hatari kiafya. Kaliforni hutumiwa hasa kama chanzo cha nyutroni

Marejeo hariri

  1. NNDC contributors (2008). Sonzogni, Alejandro A. (Database Manager) (ed.). "Chart of Nuclides". National Nuclear Data Center, Brookhaven National Laboratory. Retrieved March 1, 2010.
  2. O'Neil, Marydale J.; Heckelman, Patricia E.; Roman, Cherie B., eds. (2006). The Merck Index: An Encyclopedia of Chemicals, Drugs, and Biologicals (14th ed.). Merck Research Laboratories, Merck & Co. ISBN 978-0-911910-00-1., uk. 276
  3. Martin, R. C. (September 24, 2000). Applications and Availability of Californium-252 Neutron Sources for Waste Characterization (PDF). Spectrum 2000 International Conference on Nuclear and Hazardous Waste Management. Chattanooga, Tennessee. Archived from the original (PDF) on June 1, 2010. Retrieved May 2, 2010.
  4. Bayerisches Staatsministerium für Umwelt, Gesundheit und Verbraucherschutz: Radioaktivität und Strahlungsmessung; 8. überarbeitete Auflage, April 2006 (PDF; 1,3 MB), S. 187.
  Makala hii kuhusu mambo ya kemia bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Kaliforni kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.