Chati
Chati mabega-meupe
Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Animalia (Wanyama)
Faila: Chordata (Wanyama wenye ugwe wa neva mgongoni)
Ngeli: Aves (Ndege)
Oda: Passeriformes (Ndege kama shomoro)
Familia ya juu: Muscicapoidea (Ndege kama shore)
Familia: Muscicapidae (Ndege walio na mnasaba na shore)
Fleming, 1822
Ngazi za chini

Jenasi 5:

Chati ni ndege wa jenasi mbalimbali katika familia Muscicapidae. Siku hizi wataalamu wengi wanaainisha spishi za Thamnolaea katika Myrmecocichla.

Chati hawana rangi kali isipokuwa spishi za Thamnolaea ambao wana tumbo jekundu. Wengine ni weusi, wengine wana rangi ya kijivu au kahawia.

Spishi hizi zinatokea Afrika na kadhaa zinatokea Asia ya Magharibi mpaka Uhindi. Kwa kawaida huonekana juu ya miamba, majabali na vilima vya mawe.

Hula wadudu, matunda madogo, mafuta ya wanyama na takataka za kulika za nyumba.

Hulijenga tago lao kwa vitu vyororo kama sufu, manyoya na nyuzinyuzi juu ya uoto mfupi au kati ya mawe. Jike hutaga mayai 3-5.

Spishi za Afrika hariri

Picha hariri

  Makala hii kuhusu mambo ya biolojia bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Chati (ndege) kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.