Chris Chameleon

mwanamuziki wa Afrika Kusini

Chris Chameleon (alizaliwa 28 Julai, 1971) ni mwanamuziki wa nchini Afrika Kusini. Yeye ndiye mwimbaji mkuu na mpiga gitaa la besi wa bendi ya Boo!, [1]. Alianza kuigiza kwa mara ya kwanza katika Sonkring ya Franz Marx mwanzoni mwa miaka ya 1990, akiigiza kwenye nafasi ya 7de Laan kama mwanamuziki, [2].

Mwanamuziki Chris Chameleon
Chris Chameleon
Chris Chameleon akiwa jukwaani

Wasifu hariri

Chris Chameleon alizaliwa na Chris Mulder siku ya Jumatano, 28 Julai, 1971.

Chameleon alitoa albamu yake ya kwanza inayoitwa Ek Herhaal Jou, mwaka 2005. Inajumuisha mashairi ya Ingrid Jonker yaliyowekwa kwenye muziki. " Ek Herhaal Jou ", na albumu hiyo iliteuliwa katika tuzo ya muziki ya Afrika Kusini (SAMA) kama Albamu Bora ya Kiafrika mnamo 2006. Albamu ilifikia hadhi ya dhahabu nchini Afrika Kusini mnamo Julai 2006 na hadhi ya platinamu mnamo Desemba 2007. DVD, " Vokleur " pia ilitolewa mwaka 2005, na ilikuwa na nyimbo kutoka kwemye albamu ya " Ek Herhaal Jou " pamoja na vibao vingine kutoka bendi Boo!.

Orodha ya kazi zake za kimuziki (Diskografia) hariri

  • Ek Herhaal Jou (2005)
  • Shine (2006)
  • 7de Hemel (2006)
  • Ek vir jou (2007)
  • Flight of an Extraordinary Alien (2007)
  • Klassieke Chameleon (2008)
  • Kyk hoe lyk ons nou (2009)
  • As Jy Weer Skryf (2011)
  • Herleef (2013)
  • Posduif (2014)
  • Firmament (2016)
  • Jy en Ek en Ek en Jy (2017)

Marejeo hariri

  1. "Nakala iliyohifadhiwa". Ilihifadhi kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2019-04-03. Iliwekwa mnamo 2022-04-24. 
  2. "In conversation with Chris Chameleon". The Mail & Guardian (kwa en-ZA). 2014-10-03. Iliwekwa mnamo 2023-02-26. 
  Makala hii kuhusu mambo ya muziki bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Chris Chameleon kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.