Domobeleshi
Domobeleshi wa Sundevall (Prosymna sundevalli)
Domobeleshi wa Sundevall (Prosymna sundevalli)
Uainishaji wa kisayansi
Himaya: Animalia (Wanyama)
Faila: Chordata (Wanyama wenye ugwe wa neva mgongoni)
Nusufaila: Vertebrata (Wanyama wenye uti wa mgongo)
Ngeli: Reptilia (Wanyama wenye damu baridi na magamba ngozini)
Oda: Squamata (Mijusi, mijusi-nyungunyungu na nyoka)
Nusuoda: Serpentes (Nyoka)
Familia: Lamprophiidae (Nyoka walio na mnasaba na chata)
Fitzinger, 1843
Nusufamilia: Prosymninae (Nyoka wanaofanana na domobeleshi)
C.M.R. Kelly, N.P. Barker, M.H. Villet & Broadley, 2009
Jenasi: Prosymna
Gray, 1849
Ngazi za chini

Spishi 16:

Domobeleshi ni nyoka wasio na sumu wa jenasi Prosymna katika familia Lamprophiidae. Wamepewa jina hili kwa sababu hutumia domo lao kwa kuchimba kama beleshi.

Nyoka hawa ni wafupi, sm 45 kwa kipeo lakini sm 25-35 kwa kawaida. Rangi yao ni kijivu au kahawia mara nyingi pamoja na vidoa vyeusi au kijivubuluu. Spishi nyingine zina mabaka na nyingine zina rangi kali.

Domobeleshi huchimba katika udongo au mchanga mtifu ambapo hutafuta mayai ya mijusi na nyoka wengine. Hawaonekani sana isipokuwa wakati wa mvua.

Nyoka hawa hawana sumu kwa sababu hula mayai ya reptilia wengine tu. Kwa hivyo wanaweza kukamatwa bila shida. Lakini wakitishwa spishi kadhaa hujipinda katika zongomo na wakiguswa huzongoa na kuzonga tena upesi.

Spishi hariri

Marejeo hariri

  • Spawls, S., Howell, K., Drewes, R. & Ashe, J. (2002) A field guide to the Reptiles of East Africa. Academic Press, San Diego, CA, USA.

Viungo vya nje hariri

  Makala hii kuhusu mnyama fulani bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Domobeleshi kama uainishaji wake wa kibiolojia, maisha au uenezi wake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.