Mchanga ni punje ndogo za mwamba uliosagika.

Maji na mchanga mwambaoni

Kufuatana na mapatano ya kitaalamu mawe huitwa "mchanga" kama punje zake ziko kati ya milimita 0.063 hadi 2.

Punje hizo zinatokana na mmomonyoko wa mawe makubwa zaidi kama changarawe yaliyosukumwa na upepo au maji kwa mfano mtoni, baharini au kwenye mteremko wa mlima.

Jina mchanga halitaji mata yake lakini mara nyingi inamaanisha punje za silika (Si02) ambayo ni oksidi ya silikoni inayopatikana kwa wingi katika ganda la Dunia.

Mchanga hupatikana kwa wingi hasa kando ya bahari, jangwani au mtoni.

Mchanga ukichanganywa na saruji na maji huwa zege inayotumiwa kwa ujenzi.

Mchanga wa silika inaweza kuyeyushwa kuanzia jotoridi ya sentigredi 1713 na hivyo ni msingi wa kutengeneza kioo.

Picha hariri

Viungo vya nje hariri

 
WikiMedia Commons
Wikimedia Commons ina media kuhusu:


  Makala hii kuhusu mambo ya sayansi bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mchanga kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.