Frederick Tluway Sumaye (amezaliwa 29 Mei 1950) ni mwanasiasa wa Kitanzania ambaye alikuwa Waziri Mkuu wa Tanzania kuanzia tarehe 27 Novemba 1995 mpaka 28 Desemba 2005.

Frederick Sumaye

Fredrick Sumaye mwaka 2006
Rais Benjamin Mkapa

mhitimu wa Egerton Agricultural College (Dip)
Harvard Kennedy School (MPA)

Maisha na kazi hariri

Akiwa mwanachama wa chama tawala Chama Cha Mapinduzi (CCM), Sumaye alihudumu kama mbunge wa Jimbo la Hanang kutoka mwaka 1983 hadi 2005 na alihudumu katika Baraza la Mawaziri kama Waziri wa Kilimo, Mifugo na Ushirika. Alikuwa Waziri Mkuu kuanzia mwaka 1995 hadi 2005.

Baada ya kutoka madarakani, Sumaye alikuwa Balozi wa Shirika la Maendeleo la Viwanda la Umoja wa Mataifa; baadaye, mnamo 2006, alijiandikisha kwa mwaka kama mwanafunzi katikati ya kazi kupitia Programu ya Edward S. Mason katika Shule ya Serikali ya John F. Kennedy katika Chuo Kikuu cha Harvard, na kuwa Mwalimu wa Utawala wa Umma.

Sumaye hakufanikiwa kuteuliwa na chama tawala cha CCM kama mgombea wake wa urais mwaka 2015. Baada ya hapo, alijiunga na moja ya vyama vya upinzaji, Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), ambacho kilikuwa kati ya vyama vya upinzani ambavyo viliunda harakati za upinzani Umoja wa Katiba ya Wananchi (UKAWA) tarehe 22 Agosti 2015. Katika hotuba ambayo aliitoa muda mfupi baada ya kutangaza kwamba anajiunga na upinzani, Sumaye alisema alikuwa akifanya hivyo ili kuimarisha demokrasia.

Tarehe 4 Desemba 2019, Sumaye aliitisha mkutano na waandishi wa habari na kutangaza kuondoka CHADEMA na kuachana na vyama vya siasa kufuatia kushindwa kwake katika uchaguzi wa ndani wa nafasi ya mwenyekiti CHADEMA kanda ya Pwani. Kwa sasa tayari amekwisha kurudi kwenye chama chake cha zamani cha CCM.

Viungo vya nje hariri