3°23′S 37°33′E / 3.38°S 37.55°E / -3.38; 37.55

Picha ya Himo kwa macho ya ndege

Himo ni mji mdogo katika Wilaya ya Moshi Vijijini ya Mkoa wa Kilimanjaro nchini Tanzania.[1]

Himo huhesabiwa bado kama sehemu ya kata ya Makuyuni.

Himo iko kwenye njiapanda ya barabara T2 (Chalinze-Arusha) na T15 (Himo-Taveta). Umbali wake na Moshi ni km 29, hadi mpakani mwa Taveta ni km 15. Himo ndipo inaanza barabara ya Marangu ambayo ni sehemu ya kuanza safari ya kupanda mlima Kilimanjaro.

Ilianza kukua wakati wa kufungwa kwa mpaka baina ya Kenya na Tanzania katika miaka ya 1980 ikiwa kitovu cha biashara ya magendo.[2]

Marejeo hariri

  1. Diyamett, B.D. (2001). The Case of Himo and Its Region, Northern Tanzania. International Institute for Environment and Development. ISBN 1843690349. Iliwekwa mnamo 29 August 2012.  Check date values in: |accessdate= (help)
  2. Tacoli, Cecilia (2002). Changing Rural-Urban Interactions in Sub-Saharan Africa and Their Impact on Livelihoods: A Summary. International Institute for Environment and Development. uk. 29. ISBN 1843691876. Iliwekwa mnamo 29 August 2012.  Check date values in: |accessdate= (help)
  Makala hii kuhusu maeneo ya Mkoa wa Kilimanjaro bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Himo kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.


Isipokuwa usitaje majina ya viongozi waliopo sasa maana wanabadilika haraka mno.