Historia ya Ufini inahusu eneo ambalo siku hizi linaunda Jamhuri ya Ufini.

Historia ya awali hariri

Ufini ulikaliwa na watu tangu ilipokwisha enzi ya barafu ya mwisho, miaka 9000 KK hivi.[1] Wakazi wa kwanza walikuwa wawindaji-wakusanyaji ambao walitumia vifaa vya mawe vinavyofanana na vile vya Estonia, Russia na Norway.

Labda kilimo kilianza miaka 3000 KK - 2500 KK.[2]

Karne za kati hariri

Mwishoni mwa karne ya 13 Ufini ukawa sehemu ya Sweden hadi mwaka 1809, ilipomezwa na Dola la Russia kama ufalme mdogo wenye kujitawala kwa kiasi fulani.

Karne ya 20 hariri

Mwaka 1906, Ufini ulikuwa nchi ya kwanza duniani kuwapa wananchi wote wenye umri wa utu uzima haki ya kugombea vyeo vya serikali.[3][4]

Mwaka 1917, baada ya Mapinduzi ya Russia, Ufini ulijitangaza huru na mwaka uliofuata ukawa jamhuri baada ya vita vya wenyewe kwa wenyewe.

Wakati wa vita vikuu vya pili, Muungano wa Kisovyeti ulijitahidi kuteka Ufini wote, ukaishia kutwaa Karelia, Salla, Kuusamo, Petsamo na visiwa kadhaa tu.

Baada ya vita Ufini uliacha kutegemea kilimo ukajitosa katika uchumi wa viwanda[5] hata kufikia kuwa kati ya nchi zilizoendelea zaidi[6][7][8][9][10][11][12].

Mwaka 1955 Ufini ulijiunga na Umoja wa Mataifa ukichagua siasa ya kutoambatana na upande wowote.

Mwaka 1995 ulijiunga na Umoja wa Ulaya na mwaka 1999 ulikubali kutumia euro.

Tanbihi hariri

  1. Georg Haggren, Petri Halinen, Mika Lavento, Sami Raninen and Anna Wessman (2015). Muinaisuutemme jäljet. Helsinki: Gaudeamus. uk. 23. ISBN 978-952-495-363-4. 
  2. Georg Haggren, Petri Halinen, Mika Lavento, Sami Raninen ja Anna Wessman (2015). Muinaisuutemme jäljet. Helsinki: Gaudeamus. uk. 339. ISBN 9789524953634. 
  3. Parliament of Finland. "History of the Finnish Parliament". eduskunta.fi. Ilihifadhi kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2014-09-26. Iliwekwa mnamo 2018-02-20. 
  4. Finland was the first nation in the world to give all (adult) citizens full suffrage, in other words the right to vote and to run for office, in 1906. New Zealand was the first country in the world to grant all (adult) citizens the right to vote, in 1893. But women did not get the right to run for the New Zealand legislature, until 1919.
  5. "Finland". International Monetary Fund. Iliwekwa mnamo 17 April 2013.  Check date values in: |accessdate= (help)
  6. "Finland: World Audit Democracy Profile". WorldAudit.org. Ilihifadhi kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 30 October 2013.  Check date values in: |archivedate= (help)
  7. "Tertiary education graduation rates—Education: Key Tables from OECD". OECD iLibrary. 14 June 2010. doi:10.1787/20755120-table1. Ilihifadhi kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2011-04-30. Iliwekwa mnamo 6 March 2011.  Check date values in: |date=, |accessdate= (help)
  8. "Her er verdens mest konkurransedyktige land—Makro og politikk". E24.no. 9 September 2010. Ilihifadhi kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 14 October 2010. Iliwekwa mnamo 6 March 2011.  Unknown parameter |df= ignored (help); Check date values in: |date=, |archivedate=, |accessdate= (help)
  9. "The 2009 Legatum Prosperity Index". Prosperity.com. Ilihifadhi kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 29 October 2009. Iliwekwa mnamo 4 February 2010.  Check date values in: |archivedate=, |accessdate= (help)
  10. "Human Capital Report 2015". World Economic Forum. Ilihifadhi kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 2017-12-03. Iliwekwa mnamo 15 May 2015.  Check date values in: |accessdate= (help)
  11. "Fragile States Index 2016". Fundforpeace.org. Ilihifadhi kwenye nyaraka kutoka chanzo mnamo 4 February 2017. Iliwekwa mnamo 27 November 2016.  Unknown parameter |df= ignored (help); Check date values in: |archivedate=, |accessdate= (help)
  12. Gender Gap Report (PDF). WEF. 
  Makala hii kuhusu mambo ya kihistoria bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Historia ya Ufini kama enzi zake au matokeo yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.