Umoja wa Ulaya

muungano wa kisiasa na kiuchumi wa nchi 27 za Ulaya
Umoja wa Ulaya
Kibulgaria: Европейски съюз
Kicheki: Evropská unie
Kidenmark: Den Europæiske Union
Kieire: An tAontas Eorpach
Kiestonia: Euroopa Liit
Kifaransa: Union européenne
Kifini: Euroopan unioni
Kigiriki: Ευρωπαϊκή Ένωση
Kihispania: Unión Europea
Kiholanzi: Europese Unie
Kihungaria: Európai Unió
Kiingereza: European Union
Kiitalia: Unione Europea
Kijerumani: Europäische Union
Kikroatia: Europska unija
Kilatvia: Eiropas Savienība
Kilituanya: Europos Sąjunga
Kimalta: Unjoni Ewropea
Kipoland: Unia Europejska
Kireno: União Europeia
Kiromania: Uniunea Europeană
Kislovakia: Európska únia
Kislovenia: Evropska Unija
Kiswidi: Europeiska unionen
www.europa.eu

Umoja wa Ulaya (kifupisho: EU) ni muungano wa kisiasa na wa kiuchumi wa nchi 27 za Ulaya, baada ya Ufalme wa Muungano kujitoa tarehe 31 Januari 2020, tukio la kwanza la namna hiyo.

Ulianzishwa mwaka 1991 juu ya msingi wa Jumuiya ya Kiuchumi ya Ulaya.

Shabaha kuu zilikuwa kujenga uchumi wa pamoja, kuboresha maisha ya watu wa Ulaya na kuzuia vita kati ya nchi za Ulaya.

Nchi 19 za Umoja huo hutumia pesa moja ya Euro.

Nchi nyingi za Umoja zimepatana kufungua mipaka yao bila vizuizi kwa wakazi wote.

European Commission (Brussels)

Historia hariri

Jumuiya ya Kiuchumi ya Ulaya ilibadilisha jina lake mwaka 1992 kufuatana na mikataba ya Maastricht kuwa Umoja wa Ulaya.

Nchi wanachama zilipatana kujenga siasa ya pamoja ya kiuchumi, kifedha, kisheria na katika mambo ya nje.

Mapatano ya Schengen ilifungua mipaka ili wakazi wa nchi hizo waweze kusafiri bila pasipoti wala vibali.

Nchi 10 tena zilijiunga na Umoja wa Ulaya mwaka 2004. Mbili zaidi ziliingia 2007 na Kroatia mwaka 2013.

Wakazi hariri

Jumla ya wakazi ni milioni 447 (mwanzoni mwa 2020), sawa na 5.8% za watu wote duniani. Kuna miji 15 yenye watu zaidi ya milioni moja kila mmojawapo, kuanzia Paris ambayo inazidi milioni 10.

Upande wa lugha, lugha rasmi ni 24, lakini lugha inayotumika zaidi ni Kiingereza, kinachoweza kuzungumzwa na 51% za wakazi wote, ingawa ni lugha ya kwanza ya 1% tu. Lugha nyingine ambazo ni za kwanza kwa wananchi wengi ni: Kijerumani (18%), Kifaransa (13%) na Kiitalia (12%). Pia kuna lugha 150 hivi za kieneo.

Upande wa dini, wakazi wengi ni Wakristo (71.6%), hasa Wakatoliki (45.3%), Waprotestanti 11.1% na Waorthodoksi 9.6%. Waislamu ni 1.8%. Wafuasi wa dini nyingine ni 2.6%. Wengine 24% hawana dini au ni Wakanamungu.

Uhuru wa kuhama hariri

Kila mtu mwenye uraia wa nchi ya Umoja anaruhusiwa kuhamia nchi yoyote nyingine na kufanya kazi au biashara huko bila vibali vya pekee.

Vilevile bidhaa zote zinazotengenezwa kote katika Umoja wa Ulaya zinaweza kuuzwa katika kila nchi. Hii ni sababu ya kuwa na sheria za pamoja zinazotawala masharti ya bidhaa na uzalishaji.

Vyombo vya Umoja hariri

Halmashauri ya Ulaya hariri

Halmashauri hii ni mkutano wa viongozi wa serikali za nchi wanachama. Wanakutana mara mbili kwa mwaka na kutoa maazimo muhimu.

Nafasi ya uraisi hubadilika kila baada ya miezi 6. Ufini ilishika uraisi kati ya Julai 2006 hadi Desemba 2006, ikafuatiliwa na Ujerumani tangu Januari hadi Juni 2007.

Baraza za mawaziri hariri

Katika baraza hizi mawaziri ya Kilimo, Sheria, Mambo ya Nje hukutana na kupanga siasa ya pamoja.

Kamati ya Ulaya hariri

Hii ni kamati ya utawala inayotekeleza maazimio ya Halmashauri na bunge. Kuna makamishna 24 na mwenyekiti. Inaelekea kuwa serikali lakini haina madaraka ya serikali bado.

Bunge la Ulaya hariri

 
Bunge la Umojwa wa Ulaya huko Brussels.
 
Picha ya pamoja wakati wa kusaini mkataba wa Lisboa tarehe 13 Desemba 2007.

Bunge la Ulaya lina wabunge 751 wanaochaguliwa na wananchi kila baada ya miaka mitano.

Nchi wanachama wa Umoja wa Ulaya hariri

 CroatiaFinlandSwedenEstoniaLatviaLithuaniaPolandSlovakiaHungaryRomaniaBulgariaGreeceCyprusCzech RepublicAustriaSloveniaItalyMaltaPortugalSpainFranceGermanyLuxembourgBelgiumNetherlandsDenmarkIreland
Map showing the member states of the European Union (clickable)

Wanachama tangu 1958 (waanzilishi) hariri

Wanachama tangu 1973 hariri

Mwanachama tangu 1981 hariri

Wanachama tangu 1986 hariri

Wanachama tangu 1995 hariri

Wanachama tangu 2004 hariri

Wanachama tangu 2007 hariri

Wanachama tangu 2013 hariri

Nchi zinazoomba uanachama hariri

Jeshi la Uropa/Ulaya hariri

https://upload.wikimedia.org/wikipedia/commons/2/2c/EU_PESCO_map.svg

Tazama pia hariri

Marejeo hariri

Viungo vya nje hariri

Tovuti rasmi:

Mandhari na data:

Taarifa:

Misaada ya kufundishia:

  • European Studies Hub – interactive learning tools and resources to help students and researchers better understand and engage with the European Union and its politics.

Viungo vya nje hariri

 
WikiMedia Commons
  Makala hii kuhusu maeneo ya Ulaya bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Umoja wa Ulaya kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.