Kanisa la Biblia Tanzania

Kanisa la Biblia Tanzania (kifupi: KLB) ni kanisa la Uprotestanti lenye shirika zaidi ya 200 hasa kusini mwa Tanzania, katika mikoa ya Mtwara, Lindi na Ruvuma, lakini pia katika mikoa ya Dodoma, Dar es Salaam na Kilimanjaro. Kanisa la Biblia hufuata mtindo wa Ndugu wa Plymouth, hivyo kila ushirika unajitegemea na kanisa kwa jumla ni ushirikiano wa shirika zake. Limeandikishwa na serikali kwa namba 5881.

Kanisa la Biblia Dodoma baada ya ibada ya Jumapili.

Makao makuu yake kwa mara ya kwanza yalikuwa Mbesa (wilaya ya Tunduru). Baadaye yakahamishiwa Tunduru mjini na tangu mwaka 2024 yako mkoa wa Dodoma.

Kanisa hili lilianzishwa na wamisionari kutoka Ujerumani; tangu 1959 linaendelea kushirikiana na CMML (Christian Mission in Many Lands) hata kama utawala wa kanisa umo mikononi mwa Watanzania.

Pamoja na kazi ya kiroho KLB huendesha pia miradi ya kijamii kama vile shule, vyuo, hospitali na kituo cha kutunza watoto yatima.

Ubatizo kjijini Mbesa.

Kati ya miradi yake ni

Kuna pia miradi ya kilimo.

KLB inatoa kozi ya Biblia kwa njia ya barua (Emmaus Shule ya Biblia) na kushirikiana na Chuo cha Biblia Berea (Moshi).

Viungo vya nje

hariri
  Makala hii kuhusu dini ya Ukristo bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Kanisa la Biblia Tanzania kama historia yake, matokeo au athari zake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.