Kibosho ni jina la eneo kwenye miteremko ya mlima Kilimanjaro katika Tanzania. Wakazi wake ni Wachagga. Mwaka 2012 ni sehemu ya kata za Kibosho Kati, Kibosho Magharibi na Kibosho Mashariki katika wilaya ya Moshi Vijijini.

Katika siku za kwanza za ukoloni eneo lake lilikadiriwa kuwa na kilomita za mraba 45 zilizokaliwa na watu wengi kati ya mpaka wa msitu wa mlima Kilimajaro kwa uwiano wa mita 1650 na kutelemka hadi mita 1200 juu ya UB. Mto Karanga unapita katika nchi hii. [1]

Kwa upande wa dini Wakibosho wengi ni Wakatoliki kwa sababu wamisionari waliofika eneo hilo walijenga kanisa kubwakubwa, shule na hospitali pia. 90% ya wakazi ni wa madhehebu hayo japo kuna dini nyingine ila kwa uchache.

Kanisa Katoliki la Kibosho.

Kanisa hili la Kibosho limejengwa kwa mawe matupu, huenda ni kwa sababu lipo katikati ya Mto Karanga kushoto na Mto Nsoo kulia.

Wamangi wa Kibosho hariri

Katika karne ya 18 na 19 na chini ya ukoloni hadi uhuru Kibosho kilikuwa eneo la utemi mdogo wa Kichagga na watawala wake walijulikana kwa cheo cha "Mangi". Kuhusu Wamangi wa kwanza majina yamehifadhiwa lakini tarehe za utawala hazina uhakika. [2]

.... - .... Yansanya [1st ruler]
.... - .... Orio
.... - .... Kimboka
.... - .... Irongo
.... - .... Iweri
takr. 1810 Kirenga
takr. 1850 Kashenge
takr. 1850 - af.1862 Tatua
18.. - 18.. Ngaluma
18.. - 18.. Lokila
18.. - takr. 1872 Mamka (wa kike)
takr. 1872 - 1897 Sina
1897 - 1900 Molelia
1900 - 1911 Sianga
1911 - 1917 Malamya
1917 Barnabas Ngowi (mtendaji)
1917 - 1946 Ngulisho I (+ 1962)
1946 - 1961 Alex Ngulisho II

Mangi Sina alitawala wakati wa kufika kwa wakoloni Wajerumani. Mwaka 1889 alifaulu kumshinda Mangi Rindi wa Moshi lakini kuingilia kwa Wajerumani chini ya Hermann von Wissmann ilikuwa chanzo cha kumaliza mashindano kati ya Wamangi na utawala wa wakoloni katika Uchagga wote.

Marejeo hariri

  1. ling. makala "Kiboscho" katika Kamusi ya Koloni za Kijerumani (1920)
  2. orodha ifuatayo ni kutoka http://www.worldstatesmen.org/Tanzania_native.html
  Makala hii kuhusu maeneo ya Mkoa wa Kilimanjaro bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Kibosho kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.


Isipokuwa usitaje majina ya viongozi waliopo sasa maana wanabadilika haraka mno.