Kisiwa cha Lamu ni sehemu ya funguvisiwa la Lamu pamoja na visiwa vya Pate na Manda karibu na mwambao wa Kenya katika Bahari Hindi.

Funguvisiwa la Lamu: Lamu, Manda, Pate.
Mahali pa Lamu katika Kenya.

Kisiwani Lamu kuna mji wa Lamu na vijiji vya Shela, Kipangani na Matondoni. Shela imekuwa mahali pa utalii ambako watu wa nje wamejenga nyumba zao. Matondoni bado ni kijiji cha Waswahili watupu wanaojenga jahazi kama zamani.

Lamu inafikiwa kwa njia ya barabara ya pwani kutoka Malindi halafu kwa feri ya Mukowe. Kuna mabasi kadhaa kila siku tangu kuboreshwa kwa barabara kulipopunguza matatizo ya ujambazi njiani. Watalii wengi wanafika kwa njia ya ndege. Uwanja wa ndege wa kitaifa upo Manda kisiwani na abiria huvuka kwa maboti.

Historia hariri

Kuhusu historia ya Lamu tazama makala ya mji wa Lamu.

Picha hariri

Tazama pia hariri

Marejeo hariri