Senegal (mto)

(Elekezwa kutoka Mto Senegal)

Mto wa Senegal ni kati ya mito mirefu ya Afrika ukiwa na urefu wa kilometa 2272 pamoja na tawimto mrefu la Bafing.

Mto wa Senegal
Mto wa Senegal karibu na mdomo mjini St. Louis
Chanzo maungano ya mito ya Bafing na Bakoyé mjini Bafoulabé.
Mdomo Atlantiki
Nchi Guinea, Mali, Mauretania, Senegal
Urefu 1,790 km (2.272 km pamoja na Bafing)
Kimo cha chanzo 750 m
Mkondo 640 m³/s
Eneo la beseni 483,181 km²
Miji mikubwa kando lake St. Louis

Mto Senegal wenyewe unaanza karibu na mji wa Bafoulabe (Mali) kwenye maungano ya mito miwili ya Bafing na Bakoye ambayo yote ina chanzo huko Guinea.

Urefu wa mto Senegal ni mpaka kati ya Mauretania na Senegal. Senegal ikikaribia bahari ya Atlantiki inafika kwenye kisiwa cha St. Louis halafu inageukia kusini. Sasa inafuata pwani ya bahari ikitengwa na Atlantiki kwa kanda nyembamba ya mchanga tu hadi kuingia bahari ya Atlantiki.

Beseni la Senegal ni kilometa za mraba 483,181. Matawimto muhimu ni mto Faleme, mto Karakoro na mto Gorgol.

Mali, Mauritania, Senegal na Guinea zimeshirikiana katika mamlaka ya beseni la mto wa Senegal (Organisation pour la mise en valeur du fleuve Sénégal - OMVS).

Bonde la mto wa Senegal mpakani mwa Senegal na Mauritania.

Tazama pia hariri

  Makala hii kuhusu maeneo ya Afrika bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Senegal (mto) kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.