Ramani ya nyota ni ramani inayoonyesha nyota zinazoonekana kwenye anga wakati wa usiku. Mkusanyiko wa ramani za nyota katika kitabu kimoja huitwa atlasi ya nyota.

Ramani ya nyota katika kaburi la Misri ya Kale, takriban mwaka 1460 KK


Ramani za nyota za zamani zilionyesha mara nyingi maumbo ya kundinyota jinsi zilivyowazwa katika mitholojia ya mataifa.

Siku hizi ramani za nyota zinapatikana pia kama programu za kompyuta na katika intaneti.

Ramani za nyota zimehifadhiwa katika majengo ya Misri ya Kale tangu zamani, labda pia tangu Zama za Mawe. [1]

Majina mapya baada ya Kolumbus

Elimu ya nyota ilipanuka sana baada ya safari za upelelezi ambako mabaharia wa Ulaya walianza kuzunguka dunia yote kuanzia Magellan katika karne ya 16 BK. Hadi wakati ule elimu ya Ulaya kuhusu nyota za nusutufe ya kusini ya Dunia ilikuwa ndogo. Waarabu nao walijua tu sehemu ya nyota upande wa kusini ya ikweta. Mfano ni ramani za Albrecht Dürer alizochora mwaka 1515 (kabla ya Kolumbus na Magellan) ambako anga ya kusini lina makundinyota chache tu - na ramani ya Frederik de Wit aliyochora ramani yake miaka 150 baadaye wakati nyota za kusini zilipimwa tayari.

Ramani za kisasa

Tangu upanuzi wa elimu ya astronomia na kujulikana kwa nyota mamilioni haikuwezekana kuonyesha tena nyota zote kwenye ramani. Siku hizi ramani zilizochorwa na kuchapishwa zinatumiwa zaidi kwa kusudi la kuelimisha jamii kuhusu nyota angavu zaidi na kama msaada wa kutambua violwa kama vimondo au sayari lakini si tena kwa kazi ya kitaalamu inayotumia orodha za nyota pamoja na majiranukta angani.

  1. Whitehouse, David 2003. 'Oldest star chart' found. BBC News Science/Nature. [1] kuhusu uchoraji kwenye kipande cha meno ya ndovu wa miaka 32,000 iliyopita
  Makala hii kuhusu mambo ya sayansi bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Ramani ya nyota kama historia yake au mahusiano yake na mada nyingine?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.