Kitabu (kutoka Kiarabu كتاب, kitabun) ni mkusanyo wa kurasa zilizofungwa pamoja kwa njia ya kudumu. Siku hizi kitabu kimekuwa hasa mkusanyo wa kurasa za karatasi zilizochapishwa.

Biblia mojawapo iliyochapwa na Gutenberg. Tangu hapo Biblia imekuwa kitabu kilichoenea zaidi.
Kamusi ya Kilatini.

UNESCO imetoa elezo kuwa kitabu ni tangazo kwa umma lililochapishwa lenye kurasa zisizopungua 49.

Lakini kuna pia vitabu vyenye kurasa tupu vitakavyoandikwa kwa mkono.

Hadi karne ya 15 BK vitabu vyote viliandikwa kwa mkono kwa kutumia kalamu; kwa sababu hii vilikuwa vichache na bei ilikuwa juu.

Johannes Gutenberg alibuni mashine ya kuchapisha vitabu iliyofanikiwa na kurahisisha vitabu sana.

Siku hizi vitabu hutolewa pia kwa njia ya mtandao au CD kama vitabu pepe.

Kitabu kilichochapishwa mara nyingi zaidi duniani ni Biblia ya Kikristo: imetolewa katika nakala bilioni 5-6 hivi.

Viungo vya nje hariri

  Makala hii kuhusu mambo ya lugha bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Kitabu kama historia yake, uenezi au maendeleo yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.