Tafsiri ya Ulimwengu Mpya

Tafsiri ya Ulimwengu Mpya (kwa Kiingereza New World Translation of the Holy Scriptures) ni tafsiri ya Biblia inayotolewa na Mashahidi wa Yehova.

Historia ya tafsiri hariri

Kabla ya mwaka 1950 Mashahidi wa Yehova walitumia tafsiri nyingine zilizopatikana. Ilhali wanaamini ya kwamba makanisa yote yana kasoro nyingi[1] hawakutaka kutegemea tena vitabu vyao, hivyo walianza kutengeneza tafsiri ya kwao wenyewe kwa lugha ya Kiingereza. Agano Jipya lilipatikana mwaka 1950 na sehemu za Agano la Kale zilifuata hadi kukamilika mnamo mwaka 1960.

Tafsiri hiyo ya Kiingereza, si Biblia katika lugha zake asili (Kiebrania, Kiaramu na Kigiriki), ndio msingi wa matoleo kwa lugha nyingine zote ili kuhakikisha umoja wa madhehebu yao duniani kote.

Dibaji ya Tafsiri ya Ulimwengu Mpya ya Kiswahili inaeleza kuwa "Toleo hili la Kiswahili la mwaka wa 2017 ambalo ndilo la karibuni zaidi limerekebishwa kwa kutegemea Biblia ya Kiingereza ya Tafsiri ya Ulimwengu Mpya iliyorekebishwa mwaka wa 2013".[2]

Tabia za toleo hariri

Tabia kuu ya pekee ya tafsiri hiyo ni matumizi ya jina "Yehova" si tu kila mahali ambako Biblia ya Kiebrania inatumia YHWH lakini pia katika sehemu za Agano Jipya [3] ambapo jina hilo halipo, ila imeandikwa kwa Kigiriki Mungu au Bwana.

Kwa jumla wataalamu wa lugha na Biblia nje ya Mashahidi wa Yehova hukubaliana ya kwamba ni kosa kutamka YHWH kama "Yehova"[4].

Pamoja na hayo, wataalamu wengi wakikubaliana ya kwamba tafsiri hii kwa kawaida inatumia Kiingereza kizuri[5] bado kuna mifano mbalimbali ya kwamba matini ya Biblia ilibadilishwa kwa kusudi la kuthibisha mafundisho ya Mashahidi wa Yehova, hasa pale ambapo suala la Yesu kuitwa Mungu linaguswa.

Mifano miwili ni

  • katika Yohane 1:1 Kigiriki kinasema: "ὁ λόγος ἦν πρὸς τὸν θεόν, καὶ θεὸς ἦν ὁ λόγος". Hapa tafsiri ya Union Version kwa kukubaliana na maneno ya Kigiriki inasema "Neno alikuwako kwa Mungu, naye Neno alikuwa Mungu". Tafsiri ya Ulimwengu Mpya inatumia hapa "Neno alikuwa pamoja na Mungu, na Neno alikuwa mungu." Kuhusu Yesu inatumia "mungu" kwa herufi ndogo ili kuonyesha mafundisho yao ya kwamba Yohane hakutaka kumtaja Neno (=Kristo) kuwa "Mungu" sawa na Muumba wa mbingu na nchi bali kama "mungu" mmojawapo chini yake. Kwa Kiingereza tafsiri inatumia "a god" badala ya "God".
  • 2 Petro 1:1 Kigiriki kinasema: δικαιοσύνῃ τοῦ θεοῦ ἡμῶν καὶ σωτῆρος Ἰησοῦ Χριστοῦ; Kiswahili cha Union Version hapa ni: "haki ya Mungu wetu, na Mwokozi Yesu Kristo". Tafsiri ya Ulimwengu Mpya inasema hapa "uadilifu wa Mungu wetu na Mwokozi wetu Yesu Kristo"; inaongeza "wetu" mara ya pili kwa kufuata mafundisho yao ya kwamba "Mungu" na "Yesu Kristo" ni wawili tofauti.[6]

Marejeo hariri

  1. "Christendom", Watchtower Online library kwenye tovuti ya Mashahidi wa Yehova, iliangaliwa Septemba 2018
  2. Utangulizi, tovuti ya www.jw.org/sw, iliangaliwa Septemba 2018
  3. Mfano 2 Kor 3.16 katika Tafsiri ya Ulimwengu Mpya
  4. Jehovah, Encyclopedia Britannica 1911 online, iliangaliwa Septemba 2018
  5. Kuna ukosoaji ya kwamba tafsiri kutoka Kiingereza kwenda lugha nyingine kama Kijerumani haikuleta matokeo ya kuridhisha; hakuna utafiti wa kitaalamu kuhusu toleo la Kiswahili.
  6. John Ankerberg, John Weldon : The New World Translation of the Jehovah's Witnesses Archived 29 Oktoba 2012 at the Wayback Machine., tovuti ya Ankerberg Theological Research Institute, mwaka 2003, kupitia Wayback Machine, iliangaliwa Septemba 2018

Tafsiri ya Ulimwengu Mpya kwenye mtandao hariri

Watetezi wa tafsisi hariri

  • Stafford, Greg: Jehovah's Witnesses Defended. ISBN|0-9659814-7-9
  • Furuli, Rolf: The Role of Theology and Bias in Bible Translation: With a special look at the New World Translation of Jehovah's Witnesses, 1999. ISBN|0-9659814-9-5
  • Byatt, Anthony and Flemings, Hal (editors): 'Your Word is Truth', Essays in Celebration of the 50th Anniversary of the New World Translation of the Holy Scriptures (1950, 1953), 2004. ISBN|0-9506212-6-9
  • The Coptic Evidence
  • In Defense of the New World Translation

Maoni ya kati hariri

Wakosoaji wa tafsiri hariri

  Makala hii kuhusu mambo ya Biblia bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Tafsiri ya Ulimwengu Mpya kama historia yake au athari wake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.