Agano Jipya

Agano Jipya ni sehemu ya pili ya Biblia ya Kikristo, ikifuata Agano la Kale: Agano Jipya limefichika katika lile la Kale, na Agano la Kale limedhihirika katika lile Jipya.

Linakusanya vitabu ambavyo Wakristo wote wanaviheshimu kama vitakatifu na vilivyoandikwa baada ya ujio wa Yesu Kristo hadi mwisho wa wakati wa mitume wake.

Vitabu vyake 27 vinaleta habari zake, za mitume wake na za mwanzo wa Kanisa lake.

Vinatakiwa kusomwa kama kilele cha ufunuo wa Mungu kwa binadamu kadiri ya Historia ya Wokovu.

Jina lilitungwa na nabii Yeremia (Yer 31:30) alipotambua kwamba kwa kiasi fulani lile la mlima Sinai lilikuwa na dosari (Eb 8), lakini Mungu kwa uaminifu wake asingeweza kukubali likome tu.

Vitabu vya Agano Jipya ni kama ifuatavyo (Kwa mabano: kifupi cha kawaida kwa kutaja kitabu hiki).

Vitabu vya kihistoria

Injili nne zinasimulia habari za maisha na mafundisho ya Yesu na kutangaza hasa kifo na ufufuko wake.

Kati yake, zile tatu za kwanza zinafanana hata zikaitwa Injili Ndugu, kumbe ile ya Yohane ni ya pekee.

Historia ya mwanzo wa kanisa iko katika mwendelezo ya Injili ya Luka, jina lake

Nyaraka

Nyaraka za Paulo

Kuna maandiko 13 kati ya nyaraka yanayomtaja Mtume Paulo kama mwandishi. Wataalamu wa leo hutofautiana kama kweli nyaraka hizi zote zimeandikwa na Paulo mwenyewe. Kwa jumla saba zimetambuliwa na karibu wataalamu wote kuwa ni maandiko yake. Kuhusu mengine kuna maswali kwa sababu mbalimbali (kwa mfano tofauti za lugha, mkazo tofauti ya mafundisho), na wataalamu wengine hudai ya kuwa labda zimeandikwa na wanafunzi wake au na mwandishi kwa niaba ya Paulo.

Waebrania

  • Waraka kwa Waebrania (Ebr.) una tabia ya pekee; tangu zamani wengine waliulihesabu kuwa waraka wa Paulo ingawa ndani yake jina lake halitajwi. Leo karibu wote wanasema si ya kwake.

Nyaraka katoliki

Jina "katoliki" halimaanisha madhehebu ya Kiroma, lakini maana asilia ya neno la Kigiriki "katoliki" ambayo inaweza kutafsiriwa pia "kwa watu wote", au "zilizokubaliwa na wote".

Kitabu cha kinabii

Kitabu cha mwisho kinafuata mtindo wa kiapokaliptiko, yaani kinatazama historia kwa jumla kadiri ya imani katika ushindi wa Yesu juu ya shetani na nguvu zote za uovu. Kinaitwa

Marejeo

• Clark, Gordon (1990). "Logical Criticisms of Textual Criticism", The Trinity Foundation: Jefferson, Maryland

  • Conzelmann, Hans; Lindemann, Andreas (1999). Interpreting the New Testament: An Introduction to the Principles and Methods of New Testament Exegesis, English translation. Peabody, Mass.: Hendrickson.
  • Dormeyer, Detlev (1998). The New Testament among the Writings of Antiquity, English translation. Sheffield.
  • Duling, Dennis C.; Perrin, Norman (1993). The New Testament: Proclamation and Parenesis, Myth and History, 3rd edition. New York: Harcourt Brace.
  • Ehrman, Bart D. (2011). The New Testament: A Historical Introduction to the Early Christian Writings, 5th edition. New York: Oxford University Press.
  • Ehrman, Bart D. (2005). Lost Christianities: The Battles for Scripture and the Faiths We Never Knew. Oxford University Press. 
  • Goodspeed, Edgar J. (1937). An Introduction to the New Testament. Chicago: University of Chicago Press.
  • Levine, Amy-Jill; Brettler, Marc Z. (2011). The Jewish Annotated New Testament. Oxford: Oxford University Press.
  • Koester, Helmut (1995 and 2000). Introduction to the New Testament, 2nd edition, 2 volumes. Berlin: Walter de Gruyter.
  • Kümmel, Werner Georg (1996). Introduction to the New Testament, revised and enlarged English translation. Nashville: Abingdon Press.
  • Mack, Burton L. (1995). Who Wrote the New Testament?. San Francisco: HarperSanFrancisco.
  • Neill, Stephen; Wright, Tom (1988). The Interpretation of the New Testametnt, 1861–1986, new edition. Oxford: Oxford University Press.
  • Perkins, Pheme (2009). Introduction to the Synoptic Gospels. Eerdmans. ISBN 978-0-8028-6553-3. 
  • Schnelle, Udo (1998). The History and Theology of the New Testament Writings, English translation. Minneapolis: Fortress Press.
  • Zahn, Theodor (1910). Introduction to the New Testament, English translation, 3 volumes. Edinburgh: T&T Clark.

Viungo vya nje

 
Wikimedia Commons ina media kuhusu:

Katika lugha asili ya Kigiriki

Tafsiri ya Kiswahili

Toleo la Agano Jipya kwa Kiswahili

Maelezo ya jumla

Uandishi

  Makala hii kuhusu dini ya Ukristo bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Agano Jipya kama historia yake, matokeo au athari zake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.