Teopempto na Teona

Teopempto na Teona (walifariki 304) ni Wakristo waliofia dini yao huko Nikomedia (leo nchini Uturuki) wakati wa dhuluma ya kaisari Diokletian.

Kifodini chao.

Teotempto alikuwa askofu wa mji huo, Teona alikuwa mchawi aliyeitwa kummaliza baada ya njia nyingine ya kumuua kushindikana. Kumbe, alipoona dawa zake pia hazikumweza, alikubali kubatizwa naye. Hatimaye Teotempto alikatwa kichwa na Teona alizikwa akiwa hai[1][2][3].

Tangu kale wanaheshimiwa na Wakatoliki na Waorthodoksi kama watakatifu wafiadini.

Sikukuu yake huadhimishwa tarehe 3 Januari[4] au 5 Januari.

Tazama pia hariri

Tanbihi hariri

  1. "Serbian Orthodox Church - The Hieromartyr Theopemptus and the Holy Martyr Theonas". Serbianorthodoxchurch.net. Iliwekwa mnamo 19 April 2018.  Check date values in: |accessdate= (help)
  2. "Hieromartyr Theopemptus the Bishop of Nicomedia". Molonlabe70.blogspot.com. 5 January 2008. Iliwekwa mnamo 19 April 2018.  Check date values in: |date=, |accessdate= (help)
  3. "Hieromartyr Theopemptus the Bishop of Nicomedia". Ocafs.oca.org. Iliwekwa mnamo 19 April 2018.  Check date values in: |accessdate= (help)
  4. Martyrologium Romanum: ex Decreto Sacrosancti oecumenici Concilii Vaticani II instauratum auctoritate Ioannis Pauli P.P. II promulgatum, Romae 2001, ISBN 8820972107

Viungo vya nje hariri

  Makala hii bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Mkristo huyu, kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Je, unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuiongezea habari.